• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Jumuiya ya Wanyamapori NALIKA Wakabidhi Gawio kwa Serikali.

Imewekwa : February 15th, 2020

      Tunduru                                         15/ 02/2020

Jumuiya ya wanyamapori NALIKA  iliyopo katika wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma imekabidhi gawio kwa serikali lenye thamani ya shilingi milioni 15 kwa ajili ya kuendeleza miundombinu ya elimu katika shule tatu za sekondari za Namwinyu, Matemanga na Ligunga.

Akisoma taarifa kwa mkuu wa wilaya kabla ya kukabidhi gawio, Mwenyekiti wa jumuiya ya uhifadhi wa wanyamapori ya NALIKA Ndg Said Masoud amesema kuwa jumuiya hiyo imekuwa ikitoa gawio kwa serikali kila mwaka ikiwa ni kuunga mkono shughuli za serikali katika maeneo yanayozunguka jumuiya hiyo, na kwa mwaka huu imepanga kutoa zaidi ya milioni 30 lakini imeanza na milioni 15 kwa shule tatu kila moja shilingi milini tano  ikiwa ni kwa ajili ya kujenga hosteli katika shule zilizopo maeneo yanayozunguka jumuiya hiyo.

Akiongea na waandishi wa habari pamoja na wanajumuiya ya NALIKA,  Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mhe. Julius Mtatiro amesema serikali ina wajibu wa kushirikiana na jumuiya uhifadhi wanyamapori ya Nalika katika kufanya doria katika maeneo ya Jumuiya hiyo ili  kupambana na wahalifu wanaovamia maeneo hayo na kwamba wasisite kuomba msaada kutoka kwa serikali.

Pia Mhe. Julius Mtatiro ameitaka jumuiya hiyo kuwa na ubunifu katika kupanga mikakati ya kupata mapato ya kutosha badala ya kutegemea tuu chanzo kimoja na uwindaji na ufadhili kutoka kwa wahisani.

Alisema “jumuiya hii imeundwa mwaka 2003 ambapo mwaka 2023 itafikisha miaka 20 hivyo ni vyema kupanga mikakati endelevu ya kupata mapato nje ya shughuli ya uwindaji ikiwa ni pamoja na kujikita katika shughuli za kilimo kama kilimo cha Ufuta na Korosho ili kuweza kujiendesha”

Julius Mtatiro alisisitiza umuhimu wa kuwa na mipango ya muda mrefu ili kuepuka kuomba fedha kwa wahisani kila wakati “ nataka kuanza kuona uwekezaji wenu mkubwa kwenye mashamba ya korosho na ufuta hata katika vijiji vingine kwa kushirikiana na ofisi ya Mkurugenzi ili kupata ardhi kwa bei nafuu, na sitaki kuona taasisi ambayo ni tegemezi kwa wahisani na nitafanya ufuatiliaji”

Julius Mtatiro ametoa maagizo kwa wakuu wa shule zote tatu yaani Ligunga, Namwinyu na Matemanga kuunda kamati za usimamizi na ufuatiliaji wa fedha hizo na kuhakikisha kuwa zinafanya kazi iliyokusudiwa kwa kuzingatia kipaumbele cha shule husika ili kumaliza changamoto zilizopo kwa sasa.

Hata hivyo Mkuu wa wilaya alimazilia kwa kusema kwamba ni kweli mkakati wa wilaya ya Tunduru  ni kujenga Hosteli katika  shule zote  za sekondari wilayani Tunduru  ili kupunguza mdondoko wa wanafunzi na mimba mashuleni lakini, alisisitiza  kipaumbele kutolewa kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa ili kuweza kupokea idadi ya wanafunzi wote walipangwa kujiunga na  kidato cha kwanza mwaka 2020.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.