• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC Homera awataka viongozi ngazi ya kata na vijiji kufanya usimamizi wa miradi inayotekelezwa kwenye maeneo yao.

Imewekwa : May 14th, 2019

Mkuuu wa wilaya ya Tunduru Mhe.Juma Zuberi Homera ametoa siku sita (6) kwa mwenyekiti wa kitongoji cha Chikunja kijiji cha Angalia kilichopo Tarafa ya Lukumble mkoa wa Ruvuma kuhakikisha kuwa saruji iliyopelekwa katika kijiji hicho kwa ajili ya kujenga sakafu katika visima viwili vya maji inajengewa ili visima hivyo vifungwe pumpu na kutoa huduma kwa wananchi.

Ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa kitongoji hicho baada ya kufika kufanya ukaguzi katika shule ya msingi Chikunja na uchimbaji wa visima 2 vya maji vinavyochimbwa kupitia fedha za kuchochea maendeleo ya Jimbo kusini na taasisi ya  H.U.C (HELP FOR UNDESERVED COMMUNITY).

Mkuu wa wilaya alisema “nimesikitishwa sana na utendaji kazi wa mwenyekiti wa kitongji hiki kwani serikali imeleta saruji lakini cha ajabu miezi inaendelea tuu kupita lakini hamfanyii kazi huku wanawake wanateseka kufata maji mtoni umbali mrefu  huku shughuli nyingine zote za maendeleo zikisimama”

Niwakumbushe kuwa Mhe.Mbunge amechangia kwa kila kisima shilingi 650,000 ili kuendana na kauli mbiu ya serikali ya kumtua mama ndoo kichwani lakini kuna watu wachache wanaotaka kukwamisha jitihada zinazofanywa na serikali, hatutawavumilia kabisa.

Kwa upande mwingine mkuu wa wilaya ya Tunduru aliwaagiza wananchi wa kitongoji cha Chikunja kupanga mipango ya namna bora ya unzishwaji wa ujenzi wa zahanati kwa kuandaa benki tofali ili kupunguza kero ya kutembea umbali mrefu kufata huduma za afya, huku katika kijiji cha Azimio akiwataka kuweka mpango bora wa usimamizi wa mazao ili kuweza kupata mapato yatakayotumika katika shughuli za maendeleo ikiwa ni pamoja na kuongeza vyumba vya madarasa katika shule ya msingi Azimio.

Mkuu wa wilaya huyo alisema "wananchi wa kitongoji hiki wanasafiri umbali mrefu wa zaidi ya kilomita 20 kufata huduma za afya katika kituo cha afya Mtina, ili kukabiliana na changamoto hii kijiji mama Angalia wameshafyatua tofali 2500 kwa aili ya ujenzi wa zahanati na nyie wanachikunja mfyatue tofali ili serikali ione na kuwaletea vifaa vya kiwandani"

Aidha aliwataka wahudumu wa afya katika zahanati ya kijiji cha Azimio kutuoa huduma stahiki kwa wananchi kwani walipwa kupitia kodi za wananchi, ratiba ya utoaji huduma itolewe na ibandikwe katika mbao za ofisi za kijiji ili kuondoa usumbufu kwa wnanchi hasa siku za mapumziko na mwisho wa wiki.

Halmshauri ya Tunduru inaendelea kusimamia na kutekeleza kazi mbalimbali ili kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata huduma stahiki na kwa wakati, kwa wananchi wanaokumbana na changamoto msisite kutoa taarifa kwa serikali.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.