• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Afungua soko la Madini ya dhahabu na Vito

Imewekwa : May 29th, 2019

na Mwandishi wetu

Mkuu wa mkoa ametoa kauli hiyo jana, wakati akifungua soko la kuuzia Dhahabu na madini ya vito wilayani Tunduru ambapo alisema, kati ya fedha hizo shilingi ml 9,916, 254 zimetokana na mrabaha na shilingi ml 2.5 ni ushuru.

Mkuu wa mkoa alisema,tangu Serikali ilipoweka sheria ya kuanzishwa kwa soko la madini kumekuwa na mafanikio makubwa ikiwemo kuongezeka kwa mapato ya Serikali na udhibiti wa madini ambayo kabla ya sheria hiyo kulikuwa na vitendo vingi vya utoroshaji madini na ukwepaji mkubwa wa kodi.

Alisema, katika kipindi hicho jumla ya gram 2824.2 zimepatikana kati ya hizo gram 2540 madini ya vito na dhahabu iliyopatikana ni gram 364.2.


Aidha Mndeme,ameagiza kufanyiwa ukaguzi wa mizani na vifaa vingine vya kupima madini hasa baada ya kubaini kuwa,baadhi ya vipimo vinavyotumika haviko sahihi jambo linaloweza kusababisha udanganyifu na hivyo kuikosesha Serikali taarifa mapato halisi.


Alisema, lengo ni kufahamu thamani ya madini yetu kwani kwa muda mrefu kumekuwa na udanganyifu mkubwa unaofanywa na wafanya biashara wa madini.

Alisema, ufunguzi wa soko la madini katika wilaya ya Tunduru na Songea mkoani humo ni utekelezaji wa Agizo la Rais Dkt John Magufuri ambalo linalenga kupata uhakika wa takwimu za madini,soko na uhakika wa bei na kuondoa unyanyasaji kwa wachimbaji wadogo unaofanywa na wanunuzi.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme aliyenyoosha mkono  akiongea na baadhi ya wanunuzi wa madini ya vito  mara baada ya kufungua soko la kuuzia Dhahabu na madini ya vito wilayani Tunduru jana ambapo ameagiza madini yote yanayochimbwa katika wilaya hiyo kuuzwa katika kituo hicho badala ya kuuzwa  mitaani au nyumbani kwa wanunuzi.

Amewataka wananchi na wachimbaji wadogo wa madini katika mkoa huo kuwa walinzi wazuri wa rasiimali zetu za madini na kusisitiza kuwa yeyote atakayekamatwa anatorosha madini atachukulia hatua ikiwemo kufikishwa mahakamani sambamba na kufutiwa leseni.


Hali kadhalika mkuu wa mkoa, ameziomba taasisi za fedha ikiwemo Benki kufungua huduma za fedha katika eneo la kuuzia madini ili kuwaondolea usumbufu wanunuzi na wauzaji madini kufuata fedha mbali sambamba na kuwataka wachimbaji wadogo kuhakikisha wanafungua Akaunti badala ya kutembea na fedha nyingi mifukoni jambo ambalo ni hatari kwa usalama wao.

Awali Afisa Madini mkazi wa wilaya ya Tunduru Juma Kapela alisema, wilaya ya Tunduru imebarikiwa kuwa na madini mbalimbali ya thamani kama Dhahabu,madini ya vito na shaba.

Kapela alisema, Ofisi ya Afisa madini mkazi inasimamia jumla ya leseni hai 342 za uchimbaji mdogo na imeshapokea maombi mapya yaliyopokelewa ni 56 ya leseni za uchimbaji mdogo wa madini ambayo yapo katika hatua za kupitiwa kama yanakidhi vigezo ili yaweze kutolewa leseni.


Alisema, hadi sasa jumla ya leseni 239 zimepewa hati za makossa na leseni 1,342 zimefutwa kwa kutotimiza masharti ya umiliki wa leseni hizo kwa mujibu wa sheria.

Mkuu wa mkoa wa ruvuma akiwahutubia wananchi katika siku ya uzinduzi wa soko la dhahabu na madini ya vito wilayani Tunduru.

Alisema, kufunguliwa kwa Soko la madini katika wilaya ya Tunduru kutafungua milango kwa wachimbaji na wafanyabiashara wa madini walioko katika wilaya ya Tunduru na maeneo jirani kupata sehemu ya kuuzia na kununua madini.

Kwa upande wao wachimbaji wadogo wa madini ,wamempongeza Rais Dkt John Magufuli kwa kukubali kukutana na wadau wa sekta ya madini ili kusikiliza kero za sekta ya madini.


Hata hivyo,wameiomba Serikali iweze kutengeneza mazingira mazuri ya soko la ununuzi wa madini ya vito kwa sababu wanunuzi hao wapo katika Kampuni tofauti hivyo kukaa chumba kimoja Zaidi ya mnunuzi mmoja inaondoa usiri wa Kampuni kwa Kampuni na mchimbaji anayehitaji kuiuzia.

Makamu mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji wadogo wa Madini Mohamed Mlangwa alisema, hali hiyo inatokana na ukweli kwamba madini ya vito hayana bei maalum kama ilivyo kwa Dhahabu.

MWISHO

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.