• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

“HATUA za kisheria kuchukuliwa kwa wazazi/walezi wote ambao mpaka sasa bado hawajapeleka watoto wao shule kuandikishwa: kumpeleka mtoto shule ni takwa la kiserikali” DC Chacha

Imewekwa : February 10th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Simon Chacha ametoa maagizo hayo katika Kikao cha kujadili hali ya udahili wa wanafunzi wa kidato cha kwanza kilichofanyika leo tarehe 10.02.2025, katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Tunduru. Mhe. Chacha alitoa agizo kuwa watoto wote waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza wakaandikishwe shule mara moja.

Mhe. Chacha, ambaye alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho, ameagiza kuwa wazazi na walezi wote ambao hawajapeleka watoto wao kuandikishwa shule wanapaswa kukamatwa kuanzia kesho tarehe 11.02.2025. Alisisitiza kuwa kumpeleka mtoto shule ni takwa la kiserikali na ni kwa manufaa ya mtoto mwenyewe. Pia, wazazi/Walezi ambao wameandikisha watoto wao shule za nje ya Wilaya ya Tunduru wanapaswa kutoa taarifa haraka iwezekanavyo.

“Hatuwezi kuendelea kufanya kazi hii kwa kubembelezana, ni muda sasa wa kuchukua hatua za kisheria, hii sio kwa manufaa yao tu bali ni kwa ajili ya taifa kwa ujumla” aliendelea kuzungumza kuwa “Wanasheria wetu watatusaidia kuhakikisha tunafuata taratibu zote za kuwafikisha mahakamani wale wote watakaokaidi agizo hili”  

Aidha, Mkuu wa Wilaya ameagiza kuwa zoezi la kuwafuatilia na kuwabaini wazazi/walezi ambao hawajaandikisha watoto wao kidato cha kwanza likamilike ndani ya wiki mbili, kuanzia leo tarehe 10.02.2025, baada ya hapo zoezi hili litafuatia kwa wazazi/walezi ambao hawajapeleka kuwaandikisha watoto wao Shule ya awali na Msingi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Ndg. Chiza C. Marando alizungumza kuwa kila Mzazi/Mlezi wa Mtoto aliyefauru kujiunga na kidato cha kwanza anapaswa kumpeleka kuandikishwa.

“Watoto wote waliofauru wapelekwe shule kuandikishwa,kukosekana kwa sare za shule isiwe kikwazo cha kumnyima mtoto haki yake ya msingi, apelekwe akaandikishwe huku mzazi/mlezi akiendelea kutafuta namna ya kumpatia mtoto wake sare hizo”

Akihitimisha kikao hicho Mhe. Chacha alisisitiza kuwepo kwa ushirikiano baina wataalamu wa ngazi zote, kufanya hivyo kutawarahisishia hata katika zoezi la usimamizi wa Miradi ya maendeleo, ambapo alizungumza kuwa ataanza kuzungukia miradi yote ili kuhakikisha inakamilika ndani ya muda ulioelekezwa.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.