• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

HARAMBEE YA UJENZI WA OFISI YA CCM TUNDURU YAKUSANYA ZAIDI YA MILIONI 106 PAMOJA NA MIFUKO 15 YA SARUJI.

Imewekwa : December 29th, 2025

Wilaya ya Tunduru leo imeonesha umoja na mshikamano wa hali ya juu kupitia harambee ya kuchangia ujenzi wa Ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tunduru, iliyofanyika katika Ukumbi wa Skyway, Tunduru Mjini. 


Harambee hiyo imewakutanisha viongozi wa chama, wabunge, madiwani na wanachama kwa lengo la kuimarisha miundombinu ya chama na kuongeza ufanisi wa utendaji wake. Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mhe. Denis Masanja, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, na kupongeza mshikamano uliooneshwa na wanachama wa CCM Tunduru.

Pichani:Mhe.Denis Masanja, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru akizungumza katika Harambee.

Kupitia harambee hiyo, jumla ya Tshs. 106,055,000/- zimekusanywa pamoja na mifuko 15 ya saruji, ambapo Tshs. 28,300,000/- ni fedha taslimu na Tshs. 77,755,000/- ni ahadi. Kiasi hicho kinaonesha dhamira ya dhati ya viongozi na wanachama wa CCM katika kuhakikisha ujenzi wa ofisi hiyo unakamilika kwa wakati na kwa ubora unaostahili, ili iwe kituo imara cha kuratibu shughuli za chama wilayani.

Miongoni mwa waliochangia ni Madiwani wa CCM katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru waliotoa jumla ya Tshs. 25,000,000/-. Wengine ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Salim Abri (Asas) aliyechangia Tshs. 5,000,000/- taslimu, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi ya CCM Mkoa wa Iringa, Ndugu Ahmed Asas aliyetoa Tshs. 3,000,000/- taslimu, pamoja na Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini, Mhe. Judith Kapinga na Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini, Mhe. Mhandisi Fadhil Chilombe, kila mmoja akichangia Tshs. 5,000,000/-.

Michango mingine imetolewa na Dkt. Juma Matindana na Ndugu Saleh Kazembe waliotoa Tshs. 5,000,000/- kila mmoja, Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, Mhe. Juma Homera aliyechangia Tshs. 1,000,000/-, pamoja na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Mariam Nyoka aliyetoa Tshs. 1,500,000/-. 

Pichani: Mhe:Abdallah Mtila, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tunduru.

Aidha, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tunduru, Ndugu Abdallah Mtila, amechangia Tshs. 500,000/- taslimu na kuwashukuru wote kwa moyo wao wa kujitolea. Harambee hiyo imeacha ujumbe mzito kuwa mshikamano na ushirikiano wa wanachama na viongozi ni nguzo muhimu ya kuijenga CCM imara na kuisukuma Tunduru mbele kimaendeleo.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • HARAMBEE YA UJENZI WA OFISI YA CCM TUNDURU YAKUSANYA ZAIDI YA MILIONI 106 PAMOJA NA MIFUKO 15 YA SARUJI.

    December 29, 2025
  • MHESHIMIWA SEFU HASSAN DAUDA NDIYE MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TUNDURU

    December 05, 2025
  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.