• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Halmshauri yatoa asilimia 10 ya wanawake, vijana na walemavu.

Imewekwa : June 18th, 2019

Halmashauri ya wilaya ya Tunduru imefanikiwa kutoa mkopo kwa awamu ya pili kwa ajili ya kuwezesha wanawake, vijana na walemavu ikiwa ni utekelezaji sera ya serikali ya kuhakikisha Halmashauri kupitia mapato yake ya ndani inatenga fedha asilimia 10 kuwezesha makundi hayo.

Akitoa hotuba kabla ya kukabidhi hundi kwa makundi hayo Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Tunduru Ndg Gasper Balyomi alisema serikali inatekeleza yale yaliyopo katika sera na ilani ya chama tawala ya kuwawezesha wanawake, vijana na wenye ulemavu kiuchumi kwa kutoa mikopo isiyokuwa na Riba.

Mkurugenzi huyo alivitaka vikundi wanaokopeshwa fedha hizo kubuni miradi inayoendana na thamani ya fedha watakayopata ili iwe na tija kwa kubadilisha hali za maisha yao na familia kwani lengo ni kumuinua mwananchi kiuchumi.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Tunduru Ndg Gasper Balyomi akikabidhi hudhi kwa vikundi vya wanawake, walemavu na vijana ya asilimia 10 ya mapato ya ndani katika uwezeshaji kiuchumi.

Gasper aliwaasa vikundi hivyo kutengeneza bidhaa zenye ubora na viwango,kwa kutafuta vifungashio vizuri na lengo ili kuongeza uthamani wa bidhaa wanazozalisha.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji Ndg Balyomi aliwaagiza wataalamu mbalimbali kutembelea vikundi vijijini na kuona shughuli wanazofanya na kutoa elimu uzalishaji kwa vikundi “niwaagize wataalam wa Maendeleo ya jamii, Kilimo, Mifugo, FDC Nandembo na wengine tembeleeni vikundi vijijini kutoa elimu”

Meneja wa Benki ya NMB  tawi la Tunduru Gudluck Shirima akiongea na wanufaika wa mkopo wa asilimia kumi ya Halmashauri ambao hawapo kwenye picha kuwata kutumia fedha kujiendeleza kiuchumi.

Naye Kaimu Afisa maendeleo ya jamii Ndg Fadhili Chidyahaonga alisema kuwa Halmashauri imetoa mkopo kwa vikundi mara mbili na wanatarajia kutoa tena kwa mara ya tatu kabla ya mwaka wa fedha 2018/2019 kwisha.

Kwa upande wa meneja wa benki ya NMB tawi la Tunduru Ndg Goodluck Shirima aliviasa vikundi vinavyochukua mkopo kuwa na shunguli endelevu ili kujikomboa kutoka katika hali ngumu ya maisha, pia kufanya marejesho kwa wakati li vikundi vingine viweze kunufaika kama wao walivyopata mkopo huo.

Halmashauri ya wilaya ya Wilaya ya Tunduru kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2018/2019 imetoa mkopo kwa vikundi 24 awamu ya kwanza wenye thamani ya 33,500,000 ulitolewa na awamu ya pili jumla ya shilingi 50,363,440 umetolewa kwa vikundi vya walemavu 5, vijana 13 na wanawake 14.

Mwisho.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.