• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Fahamu Yaliyojiri Katika Mkutano wa Mwaka Jukwaa la Wanawake Tunduru

Imewekwa : September 7th, 2018

Wakiwa katika mkutano wa mwaka wa jukwaa la kuwainua wanawake kiuchumi wilayani Tunduru uliofanyika katika ukumbi wa hospitali ya wilaya, Kaimu Mkuu wa Idara ya  Maendeleo ya Jamii wilaya Bi Jocelyne Mganga  aliwataka wanawake kuwa na upendo, mshikamano na umoja ili kujiletea maendeleo kama wanawake wa wilaya nyingine.

Akizungumza na wanachama wa Jukwaa la Uwezeshaji wanawake Kiuchumi wilayani Tunduru, Mwenyekiti wa jukwaa la wanawake wilaya wakati wa kufungua mkutano wa mwaka Mama Fatuma Mkina alisema wanawake wanatakiwa kubadilika ili kuweza kujikwamua kiuchumi kwani ni muda mrefu tumekuwa nyuma.

“sisi wanawake wa wilaya ya Tunduru tumebaki nyuma kwa kipindi kirefu ni muda sasa wa kuona fursa zilizopo na kujikwamua kiuchumi, tuache hofu ya kushindwa kwani wanawake wa mikoa mingine wamewezaje!na  hata sisi tukiamua tunaweza” alisema mwenyekiti wa jukwaa.

Mama Akukweti akitoa hoja ya kufanyika  uhamasishaji  wa wanawake kujiunga na jukwaa la kuinua wanawake kiuchumi wilaya ya Tunduru katika mkutano wa mwaka uliofanyika katika ukumbi wa hospitali ya wilaya.

Akisoma taarifa katibu wa jukwaa la wanawake wilaya Bi Asigele Chonde alisema jukwaa linakumbwa na changamoto za ukosefu wa vitendea kazi, na ukosefu wa fedha kwa ajili ya kukopeshana hivyo kuchelewesha maendeleo kwa wanawake.

Bi Asigele Chonde aliendelea kutabainisha kuwa ili waweze kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa fedha jukwaa limeweka mikakati mbalimbali ikiwa ni pamoja na mchango wa shilingi 1000 kwa kila mwanamke kwa kila mwezi ambayo itawekwa katika akaunti ya jukwaa.

Na kwa upande wa mwanajukwa mama Akukweti aliwata viongozi wa jukwaa kuandaa ratiba ya kuzunguka katika kata na vijiji vyote vya wilaya ya Tunduru kufanya uhamasishaji wa wanawake kujiunga na jukwaa la wanawake, “kwani kama wilaya ya Tunduru ina takribani ya wanawake laki mbili (200,000) ni dhairi kwamba kama wote watajiunga na jukwaa mapato yatakuwa makubwa na kuwezesha kupata mikopo kwa urahisi na kuinuana kiuchumi”

wanawake wakifuatilia mkutano wa jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi uliofanyika katika ukumbi wa hospitali ya wilaya tarehe 01.septemba 2018.

Aliendelea kusema kuwa ni vyema kuwatumia hata viongozi wa umoja wa wanawake wa chama katika kata na mashina UWT  ili kuwafikia wanawake wengi zaidi.

Hata hivyo mkutano ulifikia maazimio ya kila mwanamke kuchangia shilingi 1000 kila mwezi, na ada ya kiingilio shilingi 3000 kulipwa mara moja kwa kila mwanamke/ mwanachama wa jukwaa la wanawake.


Imetolewa na 

Theresia Mallya

Afisa Habari na Mawasiliano

Halmashauri ya Tunduru

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.