• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Eng Manyanya Atoa Onyo kwa Watunza Ghala

Imewekwa : October 9th, 2018

Akiwa katika ziara ya siku moja wilayani Tunduru Naibu Waziri wa wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Eng Stella Manyanya alipokea taarifa ya maandalizi ya msimu wa korosho kwa mwaka 2018/2019 ambao umezinduliwa tarehe 01/10/2018, alisema ni vyema Bodi ya Korosho Tanzania kuhakikisha mahitaji muhimu yanapatikana kwa vyama vya msingi kwa wakati ili kupunguza malalamiko na changamoto za msimu uliopita.

Aidha Naibu waziri Eng Manyanya alitembelea  maghala manne yaliyoteuliwa kuhifadhi  korosho ghafi   kwa msimu kwa mwaka 2018/2019 ambayo ni ghala la halmashauri ya Tunduru, ghala la chama kikuu cha ushirika (TAMCU), ghala la Poa Rice Mill na ghala la forward.

Naibu waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Eng Stella Manyanya aliyevaa kitenge akitoa maelekezo kwa mkandarasi ya ufanya marekesho kwenye upandishaji wa Kuta ili kufanya mradi uwe na ubora unaotakiwa.

Vilevile naibu waziri alitembelea ujenzi wa ghala kubwa la serikali linalojengwa kwa thamani ya shilingi bilioni 5 chini ya usimamizi wa  Bodi ya Korosho Tanzania kuona changamoto zinazokabili utekelezaji wa mradi huo ambao umekuwa ukisuasua kutokana na sababu mbalimbali.

Eng Manyanya akiwa katika eneo la ujenzi wa ghala alipokea taarifa kutoka kwa mkandarasi ndugu YEKA HAMISI alisema wamekuwa wanakumbana na changamoto ikiwa ni pamoja na ucheweshaji wa fedha kutoka serikalini, ukosefu wa saruji kutokana na kiwanda cha Dangote kusimamisha uzalishaji, na masika yaliathiri kazi kwa kipindi cha January hadi machi. “tunaimba serikali kuleta fedha kwa wakati kwani changamoto kubwa imekuwa fedha kutokufika kwa wakati na zikifika ni kiwango kidogo ukilingana na tulichoomba” alisema

katika Picha ni Naibu waziri wa Viwanda, Bishara na Uwekezaji Eng Manyanya akifanya ukaguzi wa mradi unaokelezwa kwa usimamizi wa Bodi ya Korosho nchi wenye thamani ya shilingi Bilini 5. kutoka kulia ni mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh.Juma Homera, Katika ni Naibu waziri wa Eng Stella Manyanya na kushoto ni Mhandisi Yeka Hamisi.

Eng Manyanya alisema ufuatiliaji utafanyika ili fedha ziweze kuletwa kwa wakati na pia aliomba mradi wa ujenzi wa ghala kukamilika kwa wakati ili kutoa fursa kwa wananchi kutunza korosho zao katika mazingira safi na salama na kwa ubora wa hali ya juu.

Eng Stella Manyanya akitoa maagizo ya Mmoja wa watunza ghala kwa msimu wa korosho 2018/2019 ndg Forward (aliyevaa saa Mkononi) alipotembelea katika ghala lake ambalo limeteuliwa kuhifadhi korosho.

Hata hivyo Eng manyanya alitoa Onyo kali kwa watunza ghala juu ya suala la unyaufu na uchafu kama mawe na mchanga katika korosho, “seikali haitosita kuchukua hatua kwa watunza ghala ambao watasabisha usumbufu kwa wananchi au kushiriki katika suala la rushwa ili kupokea na kuhifadhi ghalani.”


Imeandaliwa na

Theresia Mallya

Afisa Habari na Mawasiliano

Halmashauri ya Tunduru

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.