• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

ELIMU hupelekea Maendeleo Endelevu

Imewekwa : February 8th, 2024

Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la uhifadhi wa Mazingira pamoja na  Wanyamapori, Protected Areas Management Solution (PAMS), wametoa Elimu kwaWanafunzi wa shule ya Sekondari Nampungu kuhusu uhifadhi wa mazingira, wanyamapori, na maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Akizungumza na Wanafunzi hao, Afisa Maendeleo ya Jamii Bi. Jecelyne Mganga aliwataka Wanafunzi hao kuzingatia Elimu na kuwa na nidhamu kwa jamii inayowazunguka. Aliwasisitiza kuachana na mambo yatakayosababisha kushindwa kutimiza malengo yao ya baadaye.

Sambamba na hilo ,Ustawi wa Jamii wakishirikiana na Dawati la Jinsia na Watoto walitoaa Elimu juu ya Ukatili wa kijinsia , na namna ya kuweza kukabiliana na ukatili huo na wapi wanaweza kwenda kupata msaada wa haraka kutoka na athari za ukatili, pamoja na haki a wajibu wa Mtoto katika Jamii.

“Elimu ni ufunguo wa Maendeleo Endelevu , tunapaswa kuizingatia  yale  tunayoyapata kutoka kwa walimu wetu”.  Alisema Bi. Mganga “Tunzeni utu wenu ,ili muweze kutimiza ndoto zenu”.

Aidha Ndg. Oscar Bakumbezi Mratibu Mradi PAMS Wilaya ya Tunduru akishirikiana na Bi. Asha, Askari wa uhifadhi kutoka jumuiya ya Chingoli na Narika Wilaya ya Tunduru Amezungumza na wanafunzi kuhusu utunzaji bora wa Mazingira na Wanyamapori.

Akizungumza na wanafunzi hao Bi. Asha alisema Elimu kuhusu uhifadhi wa mazingira na wanyamapori ni muhimu sana kwa vijana, kwani ndio watakaokuwa na jukumu la kulinda rasilimali hizi kwa ajili ya vizazi vijavyo.

PAMS inafanya kazi nzuri kwa kushirikiana na Idara ya Maendeleo ya Jamii kuwafikia wanafunzi na kuwapa maarifa na ujuzi wanaohitaji ili kuwa watunzaji bora wa mazingira. PAMS, kwa kushirikiana na Idara ya Maendeleo ya Jami pia  walikabidhi Taulo za kike kwa wanafunzi wa kike.

Mwanafunzi Zurea Ahamdi Ngaunje, kwa niaba ya wanafunzi wenzake, alishukuru Idara ya Maendeleo ya Jamii na PAMS kwa elimu iliyotolewa kuhusu uhifadhi wa mazingira, wanyamapori, na maendeleo ya jamii.pia kwa kukabidhiwa Taulo za kike zitakazowasaidia katika kutimiza ndoto zao za kitaaluma.

Ushirikiano kati ya Idara ya Maendeleo ya Jamii, PAMS, na wadau wengine wa maendeleo ni jambo la kuigwa katika kuhakikisha vijana wanapata elimu bora kuhusu mazingira na jamii

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.