• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC Mtatiro apongeza Mradi wa kilimo Kiuma

Imewekwa : October 2nd, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mh. Wakili, Julius S. Mtatiro, amepongeza mradi wa Kiuma wa Kilimo kwa kuanza kutoa mafunzo ya miaka miwili kwa vijana ili kuwawezesha kujiajiri na kuajiri wengine.

Mradi wa Kiuma wa Kilimo umeanzishwa na Taasisi ya Kiuma chini ya ufadhili wa kampuni ya kijerumani iitwayo Deichmann Company kwa lengo la kutoa Elimu biashara na kusaidia vijana wa Wilaya ya Tunduru kujikwamua kiuchumi. Mpaka sasa kwa mwaka wa kwanza wa masomo 2023/2024 vijana 42 wanaendelea kupata mafunzo.

Mradi wa Kiuma wa Kilimo unatoa mafunzo ya vitendo kwa vijana, mafunzo haya hutolewa kwa miaka miwili. Katika mwaka wa kwanza wanajifunza zaidi kilimo cha mboga mboga ambacho wanaangalia mahitaji ya mboga mboga ambazo zinazosaidia sana kuongeza lishe na virutubisho kwenye mwili wa Mwanadamu, na mafunzo ya ufugaji hutolewa mwaka wa pili wa mafunzo hayo.

“Nimevutiwa sana na mradi huu. Ni mradi wa kipekee ambao una lengo la kuwawezesha vijana kujikwamua kiuchumi. Ninaunga mkono mradi huu na nitatoa ushirikiano wa kutosha ili uweze kufanikiwa kwa ubora”. Alisema Mh. Mtatiro.

Pichani ( mwenye kofia Nyeusi): DC Mtatiro akizungumza katika ukaguzi wa Mradi wa Kiuma wa Kilimo.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Katibu Mkuu wa Taasisi ya kilimo Kiuma ndugu, Daniel Malukuta alisema mradi huo ni wa kipekee na una uwezo wa kuinua uchumi wa vijana na nchi kwa ujumla. Ambapo, wameandaa vitalu nyumba( Green House)  kwa ajili ya kilimo hicho, kilimo cha umwagiliaji na usindikaji wa chakula.

“tumeona ni bora hawa vijana tuwachukue tuwaweka hapa ili tuwape mafunzo na kuwajengea uwezo wa kuzalisha mazao mbalimbali ambayo yatawasaidia katika biashara na kuwapa ujuzi wa kufuga wanyama na samaki ili kuwapatia kipato kutokana na mahitaji ya uko mtaani”. Alisema

Alisema,katika shamba la kujifunzia kwa vitendo wameanza kuzalisha kabichi,nyanya,pilipili,bilinganya,karoti,vitunguu na bamia na katika hatua ya kwanza, vijana wanafundishwa namna ya kuandaa shamba,matuta na vitalu nyumba(green House)ambapo kupitia njia hiyo mkulima anaweza kutumia eneo dogo la uzalishaji na akilihudumia vizuri atapata mazao na mapato mengi.

Vile vile, vijana wanafundishwa kutengeneza mbolea ya mboji(asili) ambayo inatengenezwa kwa kutumia mabaki ya mimea,nyasi,mashudu ya alizeti na samadi inayochanganywa na udongo na pia mbolea ya asili ina faida nyingi kwenye uzalishaji ikiwemo kumpunguzia mkulima gharama ambayo upatikanaji wake unahitaji fedha nyingi na kusababisha baadhi ya wakulima kushindwa kumudu gharama.        

Mradi wa Kiuma  wa Kilimo ni mfano wa jinsi ya kutumia kilimo na ufugaji kusaidia vijana kujikwamua kiuchumi. Mradi huo unatoa fursa nzuri kwa vijana kujifunza ujuzi muhimu ambao unaweza kuwasaidia kuanzisha kilimo biashara wenyewe. Ambapo unatarajiwa kuwawezesha kujiajiri na kupunguza idadi kubwa ya vijana wasiokuwa na ajira Wilayani Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.