• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC Mtatiro amewataka Watendaji na viongozi kushirikiana katika usajili wa Wakulima wa Korosho

Imewekwa : February 26th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mhe.Julius S. Mtatiro, amewataka Watendaji na viongozi ngazi ya kata na kijiji kuonesha ushirikiano wa karibu kwa Makarani wanaouhuisha na kusajili taarifa za Wakulima wa korosho.

Ametoa wito huo katika kikao kazi kilichowahusisha maafisa tarafa, Watendaji wa kata, maafisa kilimo, viongozi na Watendaji wa vyama vya Msingi vya ushirika na chama kikuu cha ushirika Tunduru pamoja na baadhi ya wakulima.

Akizungumza katika kikao hicho, Meneja wa Bodi ya Korosho tawi la Tunduru, Bi. Shauri Mokiwa, amesema lengo la kikao hicho ni kuendelea kutoa msisitizo kwa viongozi na Watendaji ngazi ya serikali katika kata na vijiji kusimamia kwa ukaribu zoezi la uhuhuishaji na usajili wa Wakulima wa korosho wilaya ya Tunduru.

Aidha, Mhe. Mtatiro ameitaka Bodi ya Korosho Tanzania kuendeleza zoezi hili mpaka Machi 31, 2024 kutokana na ukubwa wa eneo la Wilaya ya Tunduru ukilinganisha na maeneo jirani ambapo zoezi hili linafanyika pia. amewataka Wakulima wa korosho kuonesha ushirikiano na kujitokeza kwa wingi ili kukamilisha zoezi hilo kwa wakati.

“Uchumi wetu ni  mazao , hususani zao la korosho, tushirikiane katika kutimiza zoezi hili ”. Alisema Mhe. Mtatiro

Sambamba na hayo, DC Mtatiro amevipongeza vyama vya Ushirika vya Msingi na Chama kikuu cha Ushirika Tunduru (TAMCU) kwa kuonesha utendaji kazi mzuri, pia ameviomba kuwa mabalozi wa zoezi hili kwa wakulima katika maeneo yao husika.

Wilaya ya Tunduru inakadiliwa kuwa na zaidi ya Kilometa za Mraba 18,000 ,ambapo shughuli kubwa ni kilimo hasa zao la korosho, ambapo kwa msimu uliopita Wilaya ya Tunduru ilifanikiwa kukusanya zaidi ya Tani 25,000 za Korosho.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.