• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC Mtatiro akagua uendeshaji Maghala ya Korosho.

Imewekwa : December 22nd, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mhe. Julius S. Mtatiro, amefanya ziara ya kawaida ya kukagua uendeshaji wa maghala ya kuhifadhia korosho katika wilaya hiyo Disemba 22, 2023.

Ziara hiyo iliyoambatana pamoja na kamati ya Ulinzi na Usalama, Chama Kikuu cha Ushirika, wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, ilifanikiwa kutembelea maghala 7 yaliyopo katika Halmashauri ya wilaya ya Tunduru ambayo yanahifadhi Korosho.

Akizungumza baada ya ziara hiyo, kuelekea mnada wa Mwisho wa zao la Korosho Wilayani Tunduru,Mhe. Mtatiro aliagiza kuundwa Kwa kamati ndogo ya wataalamu ili kuendelea kukagua na kuhakikisha kuwa maghala yote 7 yamezingatia miongozo ya kuhifadhi na kusafirisha korosho katika magunia yenye ujazo si chini ya kilo 80, ambapo hii itasaidia kulinda ubora wa soko la zao hilo na kuongeza thamani yake.

Mhe, Mtatiro amesisitiza, kuendelea kulinda uchumi wa zao hili kwa kuhakikisha kuwa korosho zinasafirishwa kwa njia sahihi na zinapelekwa kwa wanunuzi zikiwa katika ujazo na ubora unaohitajika na wanunuzi wa zao hilo.

“Korosho ni zao muhimu sana la biashara nchini Tanzania, linasaidia kuingiza fedha nyingi za kigeni, hivyo, yatupasa kulisimamia kwa kufuata miongozo iliyopangwa ili kuweza kulinda ubora wake”. Alisisitiza.

Akiwa katika ziara hiyo, Mhe. Mtatiro alipata wasaa wa kuzungumza na watendaji pamoja na wenyeviti wa vyama vya msingi (AMCOS) ambapo Mhe, Mtatiro, alisisitiza umuhimu wa AMCOS kuwalipa wakulima kwa wakati, kwani  itasaidia kuongeza motisha kwa wakulima kulima korosho kwa wingi.

Aidha Mhe. Mtatiro amepongeza vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS) ambavyo vimekuwa vikichapa kazi vizuri katika kuhifadhi na kusafirisha korosho, amewataka vyama hivyo kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha kuwa korosho za Tanzania zinapata soko la uhakika na wakulima wanapata bei nzuri.

 Katika ziara hiyo, watendaji nane katika maghala matatu walishikiliwa na vyombo vya usalama Kwa ajili ya maelezo zaidi, kwasababu ya kutoonesha uaminifu katika utunzaji na usafirishaji wa zao hilo kwenda kwa wanunuzi

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.