• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC MASANJA asisitiza uwajibikaji kwa watumishi wa afya Tunduru.

Imewekwa : August 14th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mhe. Denis Masanja, amefanya kikao na watumishi wa idara ya afya ambapo amewataka kuwa wajibu, kujitolea, na kuwatumikia wananchi kwa uaminifu na weledi wa hali ya juu. Kikao hicho kililenga kuboresha huduma za afya katika wilaya ya Tunduru.

Katika hotuba yake, Mhe. Masanja alisisitiza masuala mbalimbali muhimu yanayohusu utoaji wa huduma bora. Alianza kwa kusisitiza umuhimu wa uwajibikaji na utoaji wa huduma bila kuchelewa. "Kila mmoja awajibike, tujitoe. Tumekuja kuwatumikia wananchi. Hatutaki kusikia manung’uniko ya kuchelewa kutoa huduma Pamoja na changamoto zinazoweza kusababishwa na mtandao na mfumo bado tujitahidi kuhakikisha tunatoa huduma kwa haraka bila kuchelewa wakati tukitatua changamoto hizo" alisema.

Vilevile, aligusia suala la usalama wa taarifa za wagonjwa, akisisitiza kuwa ugonjwa ni siri kati ya mgonjwa na muuguzi wake. "Nina Imani Usalama wa taarifa za wagonjwa utazingatiwa muda wote," alieleza.

Mhe. Masanja pia alisisitiza suala la usafi wa mazingira ya vituo vya afya, akisisitiza kuwa ushiriki wa watumishi katika zoezi la usafi ni jambo la lazima. Kuhusu mavazi, aliwataka watumishi kuvaa kwa kufuata miongozo iliyowekwa ili kuleta heshima na utambulisho wa taaluma.

Ili kuboresha utoaji wa huduma na kujitathmini, Mhe. Masanja alitoa maelekezo ya kuanzishwa kwa kitengo cha kupokea malalamiko na kuweka masanduku ya maoni. Alisema hatua hii itasaidia kujua kiwango cha kuridhika kwa wananchi na huduma zinazotolewa. "Hii itatusaidia kujua kiwango cha utoaji huduma na kujitathmini," aliongeza.

Akizungumzia suala la upatikanaji wa dawa, Mkuu wa Wilaya alisisitiza kuwa malalamiko ya wananchi kuhusu ukosefu wa dawa yanapaswa kushughulikiwa haraka. Aliongeza kuwa ni muhimu kuweka mikakati ya utoaji elimu kwa wananchi kuhusu Magonjwa ya mlipuko na magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza kama vile Kipindupindu, Mpox, Kisukari, Magonjwa ya moyo na shinikizo la damu na mengineyo.

Mhe. Masanja alikumbusha kuwa Wilaya ya Tunduru ina changamoto ya mwingiliano mkubwa wa watu kutokana na eneo lake la mpakani, barabara kuu, uchimbaji wa madini, na kilimo cha mikakati. Hali hii inahitaji weledi na umakini wa hali ya juu katika kutoa huduma za afya.

Mwisho aliwapongeza kwa huduma nzuri za Afya wanazotoa na kuwataka kuzingatia maelekezo yake ili tuendelee kutoa huduma bora kwa wananchi.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.