• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

COUNSENUTH yahitimisha mradi wa Kijana Jiongeze awamu ya pili.

Imewekwa : August 15th, 2024

Asasi ya kiraia COUNSENUTH ambao ni wasimamizi wa utekelezaji wa mradi wa Kijana Jiongeze kwa kushirikiana na Halmashauri kupitia ufadhili wa MasterCard Foundation imefikia tamati kwa awamu ya pili ya mradi huo, huku wakikabidhi vifaa vya michezo na taaluma (Kamusi na Jezi) ili kuendelea kuinua sekta ya michezo pamoja na Elimu kwa shule 23 za Sekondari zilizopo Wilayani Tunduru.

Akizungumza katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mheshimiwa Simon Chacha ambaye alikuwa mgeni rasmi, aliipongeza asasi hii kwa kuendelea kuwa miongoni mwa wadau ambao wanameweza kusaidia kuinua Sekta ya Elimu katika Wilaya ya Tunduru.

“Niwapongeze kwa kuweza kumaliza awamu yenu ya pili ya mradi huu wa Kijana Jiongeze, pamoja na mafanikio tuliyonayo kama Wilaya katika sekta hii ya Elimu, lakini bado tunawahitaji, tutashukuru sana kama mkiendelea kuwa nasi kwa awamu nyingine tena” Alisema “Tunawashukuru kwa kuwa mchango mkubwa katika kuinua ufaulu wa wanafunzi wetu”.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi ya kiraia COUNSENUTH Bi. Shakila Mayumana ameeleza kuwa, wameweza kupata mafanikio makubwa kupitia mradi huu, ikiwemo kuongeza ufaulu katika Shule ambazo walizifikia, kupunguza utoro wa wanafunzi, wameweza kusaidia watoto kujitambua na pia wameweza kuanzisha bustani za mboga mboga na matunda, kuhamasisha michezo na vile vile mradi huu umewezesha kuanzishwa na kuboreshwa klabu mbalimbali zilizoko mashuleni kwa  mfano Kijana Jiongeze, klabu za Ushauri wa kitaaluma (Career guidance and councelling Club), kuboresha mahusiano kati ya mwalimu na mwanafunzi, pamoja na kuongeza ushiriki wa wazazi hasa kwenye masuala ya elimu.

Aidha, Bi. Shakila alitumia fursa hiyo kuwaomba Walimu, Halmashauri na Wilaya kwa ujumla kuendeleza shughuli na mafanikio yaliyoletwa na Mradi wa Kijana Jiongeze ili uwe endelevu.

Mradi wa Kijana Jiongeze kwa awamu ya pili iliyoanza mwaka 2021 mpaka 2024 umeendelea kushirikiana na Idara ya Elimu Sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, umefanikiwa kuzifikia Shule 23 za Sekondari ambazo zina wanafunzi kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne.

COUNSENUTH kwa kushirikiana na Idara ya Elimu Sekondari ya Wilaya ya Tunduru imetekeleza mradi wa KIJANA JIONGEZE wenye lengo kuu la kukabiliana na changamoto za ufaulu wa na kuhusisha njia za kuwawezesha wasichana kuwa na stadi za maisha zitakazowasaidia kutambua uwezo wazo, kujiamini na kuwaandaa kwa ajili ya ajira na kujiajiri. Mradi huu umetekelezwakwa awamu zote mbili katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, kwa ufadhili wa MasterCard Foundation.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.