• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

CHAWISI YASHEREHEKEA Historia Mpya – Zahanati Mpya Yazinduliwa, Nyumba Ya Mtumishi Kukamilika Hivi Karibuni.

Imewekwa : September 1st, 2025

  Tarehe 31 Agosti 2025, Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ilizindua rasmi utoaji wa huduma katika zahanati ya kijiji cha Chawisi. Zahanati iliyojengwa na Serikali ya Awamu ya Sita kwa gharama ya shilingi milioni mia mbili tisini na tatu, laki saba na hamsini elfu.

Ni siku ya furaha, siku ya historia, na siku ambayo wananchi wa Chawisi wataikumbuka daima. Kwa muda mrefu, walitembea umbali mrefu kutafuta huduma za afya, lakini sasa huduma hizo zimeletwa mlangoni mwao. Furaha na shangwe za wananchi wa Chawisi zimesikika kila kona. Mwenyekiti wa kijiji hicho, kwa niaba ya wananchi wote, ametoa shukrani za dhati kwa serikali ya awamu ya sita kwa mradi huu mkubwa unaogusa maisha ya kila mmoja wao.

Lakini sio zahanati pekee – nyumba ya mtumishi pia ipo hatua za mwisho kukamilika, ishara ya kwamba huduma hii itakuwa ya kudumu na ya uhakika.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, Mganga Mkuu wa Wilaya, Dkt. Wilfred Rwechungura, aliwataka wananchi wa Chawisi kujitokeza kutumia huduma zote zitakazotolewa katika zahanati hiyo. Aliwaelekeza wajawazito kuhudhuria kliniki pamoja na wenza wao, na watoto chini ya miaka mitano kupewa chanjo zote muhimu, dawa kinga na ushauri wa kiafya. Kwa kufanya hivyo, alisema, tutapunguza vifo vya uzazi na vifo vya watoto wachanga.

Aidha, Dkt. Rwechungura alisisitiza umuhimu wa kujikinga na magonjwa ya kuambukiza kama vile malaria, kifua kikuu, UKIMWI na homa ya ini. Vilevile aliwataka wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu na Mpox, kwa kuzingatia kanuni za usafi: matumizi ya vyoo bora, kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni, na kuhakikisha maji ya kunywa ni safi na salama.

Mwisho, aliwakumbusha wananchi kuilinda miundombinu ya zahanati yao, huku akiwataka watumishi kutoa huduma bora na rafiki kwa kila mmoja, wakiwemo vijana.

Zahanati ya Chawisi si tu jengo jipya, bali ni ishara ya dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan – dhamira ya kupeleka maendeleo yanayoonekana hadi ngazi ya kijiji, dhamira ya kugusa maisha ya wananchi moja kwa moja.

Leo Chawisi inasherehekea, kesho itakuwa kijiji kingine, na hatua kwa hatua, Tanzania yote inasogea mbele – kwa afya bora, maisha bora na maendeleo yanayoguswa na kila mwananchi.

Hakika, Serikali ya Awamu ya Sita – Maendeleo Yanayoonekana, Matokeo Yanayoguswa!

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.