• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

BODI ya lishe Tunduru yazinduliwa.

Imewekwa : October 27th, 2023

Bodi ya Afya na kamati za usimamizi wa vituo vya kutolea huduma ya Wilaya ya Tunduru imezinduliwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mheshimiwa, Wakili Julius S. Mtatiro tarehe 27.10.2023. Uanzishwaji wa Bodi hii ikiwa ni kutimiza takwa la Sera ya Wizara ya Afya katika kuboresha utoaji wa huduma za Afya nchini.

Bodi ya Afya na kamati za usimamizi wa vituo vya kutolea huduma ya Wilaya ya Tunduru ilianzishwa Mwezi Januari 2023 huku ikifuata hatua zote za uanzishwaji, ikiwa na wajumbe 18, wakiwemo wataalamu wa afya, viongozi wa jamii, na wawakilishi wa wananchi.

Akizungumza Katika uzinduzi huo, Mh. Wakili Mtatiro, Alisema, Bodi hiyo itasaidia Halmashauri kusimamia ufanisi wa shughuli za afya na kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi wa Tunduru. Pia, Mh. Wakili Mtatiro alisisitiza Bodi kusimamia nidhamu za watumishi wa afya na kuhakikisha kwamba wanatekeleza majukumu yao kikamilifu. 

“Kazi ya bodi hii ni kusimamia fedha za Halmashauri ziende katika vipaumbele vilivyopangwa na Halmashauri pamoja na Baraza la madiwani, na pale ambapo Bodi ikigundua kuna fursa ambayo inaweza ikapanua wigo wa mapato msisite kushauri na kusimamia hilo Alisema, Mnapaswa kuhakikisha fedha zetu haziendi sehemu tofauti, madawa yanaponunuliwa yaende kwa walengwa yasitoke vituo vya kutolea huduma kwenda maduka ya watu binafsi.

Aidha, Mhe. Mtatiro alitilia mkazo juu ya wananchi kupatiwa Elimu ya mfuko wa Huduma za Afya (CHF) iliyoboreshwa, ikiwa ni hatua muhimu katika kuboresha upatikanaji na ubora wa huduma za afya kwa wananchi wa kipato cha chini.

Uzinduzi wa Bodi hiyo ni hatua muhimu katika kutekeleza sera ya Wizara ya Afya ya kuboresha utoaji wa huduma za afya nchini. Bodi hiyo inatarajiwa kuchangia katika kuboresha ufanisi wa shughuli za afya katika Halmashauri, pamoja na kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi wa Tunduru.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.