• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

BODI YA KOROSHO YAIPA KIPAUMBELE TUNDURU

Imewekwa : May 29th, 2017

         

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh Juma Homera wakati akitoa salamu za serikali katika mkutano wa baraza la madiwani uliofanyika katika ukumbi wa klasta wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma.

Aidha aliendelea kusema kuwa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru imechuguliwa na bodi ya korosho kama sehemu ambayo watajenga ghala la kisasa la kuhifadhia korosho na mpaka sasa taratibu za ujenzi zinaendelea kwa kusafisha eneo la ekari kumi tayari kuanza ujenzi huo mara moja.

Aidha Mh Homera alisema kuwa  pembejeo za korosho mwaka huu zitatolewa bure kwa wakulima ambao watapalilia mikorosho hivyo kuwataka wananchi kufanya palizi katika mashamaba ya mikorosho.

Vilevile alitaka haki kutendaka katika ugawaji wa pembejeo za korosho ili kuondoa malalamiko kwa wananchi, na kusisitiza kuwa viongozi wa vijiji na kata kusimamia kwa karibu ila kila mkulima wa korosho ajiandikisha mapema.

Hata hivyo Mh Homera aliwataka wahesimiwa madiwani kutumia kamati ya maendeleo ya kata kuibua miradi mbali mbali ya maendeleo, vyanzo vya mapato, ujenzi wa matundu ya vyoo, madarasa ili kuboresha miundombinu  katika maeneo yao ya uongozi.

“tumieni mabaraza ya kata kuibua miradi ya maendeleo, pangeni mkakati wa kupunguza matatizo ya katika shule kama ujenzi wa nyumba za walimu, madarasa na matundu ya vyoo”

Vile vile alikumbushia suala la ukusanyaji wa mapato kusimamiwa  na kufuatiliwa kwa weledi hasa katika maeneo ya stand na sokoni, kwani kuna baadhi ya magari ya kwenda vijiji yanapaki nje ya standi ili kukwepa kulipa ushuru.

“Niwaombe Halmashauri hasa idara inayosimamia mapato kuangalia kwa ukaribu watu wanaokwepa ushuru na kutenga eneo kwa ajili ya kupaki magari madogo ili kuweza kukusanya mapato yanayopotea” alisema Mh Homera.

Sambamba na hayo aliwataka madiwani kushirikiana na wataalam katika kutekeleza miradi ya maendeleo inayopelekwa katika Kata zao na pia kamati ya fedha kukosoa dosari zinazoonekana katika miradi ya maendeleo.

“serikali haitakaa kimya kwa mtendaji yeyote atakayeshindwa kutekeleza wajibu wake na itawashughulikia Wakuu wa Idara atakayeshindwa kutekeleza wajibu wake kwa Umma” alisema mkuu wa wilaya.

Aliendelea kusemakuwa kuna udanganyifu unaofanywa na vyama vya msingi kwa kutotumia kibali cha ununuzi wa mazao kutoka Halmashauri, na baadhi yao wanasafirisha mazao kwa kutumia mabasi hivyo kuwataka waache mara moja.

Homera alisema kuna chama cha msingi cha SAM waliosafirisha mbaazi gunia 20 kupitia basi na kumuomba Afisa Ushirika Wilaya kuwachukutulia hatua za haraka na kukifuta chama hicho cha msingi mara moja kwa kukiuka sheria za ushirika.

Theresia mallya.

Afisa Habari (w)


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.