• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

BARAZA la madiwani robo ya nne Tunduru.

Imewekwa : August 28th, 2023

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru wamefanya baraza la robo ya nne kwa mwaka wa fedha ulioishia juni 2023 tarehe 27/08/2023 katika ukumbi wa mikutano claster uliopo Tunduru.

Mkutano huo wa baraza ulihudhuriwa na Waheshimiwa Madiwani , Mkuu wa wilaya ya Tunduru ,Mkurugenzi mtendaji, Ofisi ya RAS ,Wakuu wa idara na vitengo na Maafisa tarafa.

Akizungumza, Mwenyekiti wa mkutano Mheshimiwa Hairu Mussa ambaye ni Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Tunduru , ameishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa ,Dkt. Samia suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa ya kuendelea kuinua maendeleo katika wilaya ya Tunduru.

"Tunaishukuru serikali kwa kutuletea miradi mingi ambayo haijawahi tokea kwa kipindi cha nyuma". Alisema.

Aidha Mheshimiwa Hairu amewasisitiza wataalamu ,kuzidi kusimamia zoezi la ukusanyaji wa mapato kwa ukaribu ili kuongeza mapato, ambayo yanakwenda kukamilisha miradi yetu ya maendeleo iliyopo katika kata na vijiji.

Vile vile amesisitiza idara ya kilimo maafisa ugani kuwa na karibu na wakulima ,ili kuweza kuwasaidia mbinu bora za kuweza kuongeza uzalishaji, hasa katika mazao haya ya biashara katika wilaya yetu ya Tunduru.

Aidha, Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mheshimiwa Julius Mtatiro, amesisitiza katika kuongeza vyanzo vya mapato katika Halmashauri ya wilaya ya Tunduru , na kuangalia fursa mpya zitakazoweza kuongeza ukusanyaji mapato katika Halmashauri ya wilaya ya Tunduru.

Vile vile Mhe. Mtatiro amewataka madiwani kusimamia kwa ukaribu suala la ufugaji holela wakishirikiana na watendaji wao wa maeneo hayo, ikiwa ni pamoja na kuwahimiza wananchi kutouza maeneo yao yanayosababisha kukaribisha ufugaji holela katika wilaya yetu.

"Ninyi ni wawakilishi wa wananchi katika maeneo yenu,tukaongeze nguvu ya mikutano na watendaji wetu, tusaidiane kusimamia ili kuondoa ufugaji holela " alisisitiza Mhe. Julius Mtatiro.

Baraza la madiwani liliambatana na uchaguzi wa viongozi ngazi kuu tatu,kamati ya maadili ambayo itaongozwa na Mh. Hamisi Kaesa Diwani wa kata ya Matemanga, kamati ya Uchumi itaongozwa na Mh. Ado Saidi Tima Diwani kata ya Mchesi, na kamati ya huduma za jamii itaongozwa na Mh. Stawa Timamu Diwani viti maalumu kata ya Matemanga.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda,Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.