• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WAFAHAMU NINI JUU YA BIMA....?

Imewekwa : March 16th, 2018

WANANCHI WILAYANI TUNDURU WAPATA ELIMU YA BIMA.

Miaka mingi iliyopita kipindi cha wakoloni wakati wananchi wengi nchini Tanzania na duniani kote wakiwa katika wimbi la kupata hasara za upotevu na uharibifu wa mali zao na kupata matatizo makubwa ya kiafya ambapo matibabu yake ni vigumu kuyamudu kutokana na kughalimu pesa nyingi ulitokea ufumbuzi wa matatizo hayo kwa kuanzisha mifumo ya ukataji bima.

Katika kuhakikisha Elimu ya bima inawafikia wananchi wengi zaidi, Mamlaka ya usimamizi wa shughuli za bima nyanda za juu kusini wametoa Elimu  ya masuala ya bima wilayani Tunduru hapo jana.  Akifungua mafunzo hayo yaliyohudhuriwa na mamia ya wananchi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji  Halmashauri ya Wilaya  Tunduru Bw. Eberhad Halla aliwasihi wananchi kujiunga na makampuni ya bima mbalimbali za afya, biashara, mali zao  ili kupunguza makali ya maumivu pindi wanapopata majanga ya mali hizo.

Naye meneja  wa Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima nyanda za juu kusini   Bi. Consolata M. Gabone alianza kwa kufafanua kwa kina maana ya bima kuwa, ni mkataba wa biashara ambapo mtu mmoja, ama kikundi cha watu, taasisi au shirika, kwa mujibu wa sheria, huchukua jukumu la kutoa ahadi ya kulipa hasara itakayotokana na uharibifu wa mali, upotevu wa mali, kifo, au hasara nyinginezo anazopata mkataji wa bima anayeingia mkataba na mtoaji wa bima yaani yule anayekubali kuwa tayari kufidia hasara hiyo. Akiendelea kueleza aina na umuhimu wa  Bima, meneja huyo alisema "

Bima imegawanyika katika makundi mawili:-

i)Bima za muda mrefu: Hizi ni bima ambazo muda wake ni zaidi ya mwaka mmoja na kuendelea, mfano bima za maisha na

ii)Bima za muda mfupi; hizi ni bima ambazo ni mikataba ya muda usiozidi mwaka mmoja, mfano: bima za magari, moto, meli, ndege, wizi na ajali."

"Bima zote za muda mrefu na muda mfupi ni muhimu sana maishani mwetu kwani kuna bima za aina nyingi mfano bima za vyombo vya moto, bima za biashara, bima za afya, bima za maisha, bima za kilimo, bima za moto na bima za ajali kazini. Bima hizi zinasaidia kwanza kabisa kulinda biashara kutokana na majanga yasiyo tarajiwa, pili kulinda wafanyakazi kutokana na majanga mbalimbali, tatu kulinda afya ya mkataji wa bima, nne kulinda wateja ambao wanaweza kudhurika katika eneo la kazi na mwisho kuleta mazingira bora ya kufanya kazi katika biashara." Alisema Bi. Consolata Gabone

Bwana Kurenje Mbura ambaye ni afisa mafunzo ya bima alisema serikali kutokana na umuhimu wa bima na baadhi ya matatizo yaliyokua yanajitokeza kwenye utoaji wa huduma za bima mwaka 2009 serikali ilifanya marekebisho ya sheria ya bima na kuunda sheria mpya ya bima namba 10 ya mwaka 2009 ndipo kikaundwa chombo maalumu kinachojitegemea kikiwa chini ya Wizara ya Fedha na Uchumi cha kusimamia na kudhibiti masuala ya bima kiitwacho Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima (Tanzania Insurance Regulatory Authority "TIRA")  inayoongozwa na Kamishina wa Bima Nchini. Chombo hiki kiliundwa ili Kuweka mazingira mazuri ya ushindani katika soko la bima hapa nchini, Kusajili wadau mbalimbali wanaofanya biashara za bima (Kama vile, Makampuni ya Bima,Madalali wa Bima,Wakadiriaji hasara za mali na Ajali; na Mawakala wa Bima), Kuindeleza sekta ya bima na kuifanya kuwa kichocheo cha kukua kwa uchumi, Kuweka viwango vya kiutendaji wa kibiashara ndani ya soko la bima, Kuhakikisha soko la bima hapa nchini haliingiliwi, Kuhakikisha kuwa huduma zitolewazo ni za gharama nafuu na zinazomlenga mteja, Kushughulikia malalamiko ya wananchi kuhusiana na huduma za bima na Kutoa elimu ya bima kwa umma.

 Ili kuhakikisha kuwa elimu  na huduma ya bima inawafikia wananchi wengi zaidi nchini Tanzania mamlaka hiyo imegawa kanda za usimamizi. Kwa Zanzibar ofisi ipo Zanzibar na kwa Tanzania bara mamlaka ina ofisi tano ambazo ni Kanda ya Nyanda za Juu Kusini- Mbeya, Kanda ya Ziwa- mwanza, Kanda ya Kati- Dodoma, Kanda ya Kaskazini- Arusha na Makao Makuu ya Mamlaka ya Bima Dar es Salaam.

Kwa sasa wananchi wanaweza kupata taarifa mbalimbali za mamlaka ya usimamizi  wa shughuli za bima na kuhakiki stika za bima za vyombo vya moto kirahisi zaidi kupitia simu zao za mkononi kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi, kupakua App ya TIRA MIS na njia ya mwisho ni kutumia mtandao wa http//mis.tira.go.tz

Bw. Kurenje mbura Afisa mafunzo ya bima akijibu maswali yahusuyo bima (aliyesimama) na kulia kwake ni meneja wa mamlaka ya usimamizi wa bima nchini kanda ya nyanda za juu kusini Bi.Consolata Gabone



Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.