• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

ZIARA ya Naibu Waziri wa Maji Tunduru.

Imewekwa : November 21st, 2023

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Eng. Maryprisca Mahundi (Mb), amekagua miradi ya maji kwa siku mbili kuanzia tarehe 20-21 mwezi Novemba katika wilaya ya Tunduru, mkoani Ruvuma.

Akizungumzia hali ya upatikanaji wa maji katika mji wa Tunduru, Mhe.Eng.Mahundi amepongeza juhudi zinazofanywa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) katika kutekeleza mradi huo. Hata hivyo, ameonyesha kutoridhishwa na kasi ya usambazwaji wa maji kwa maeneo ya mjini Tunduru, amemtaka Meneja wa Usambazaji wa Maji Tunduru mjini, kushughulikia changamoto zote zinazokwamisha upatikanaji wa maji na kuzitafutia ufumbuzi wa haraka.

Katika ziara hiyo, Mhe. Eng. Mahundi alikagua mradi wa maji uliopo katika Tarafa ya Nalasi unaosimamiwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA). Mradi huo unagharimu shilingi Bilioni 2.4 na una uwezo wa kuhudumia wananchi kutoka vijiji 7. Ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia 70, ambapo hadi kufikia sasa, kilomita 3 kati ya 24 za mabomba ya kusafirisha maji kutoka kwenye chanzo cha maji hadi vijijini zimeshakamilishwa. Aidha, vituo 9 kati ya 24 vya maji vimeshajengwa.

Akizungumza na wananchi, amesema kuwa Serikali ina dhamira ya kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata maji safi na salama. Hata hivyo, amesisitiza kuwa ni lazima wananchi wote wanashirikiana na kuelimishana juu ya umuhimu wa kutunza miundombinu ya maji. Pia, kuwahakikishia kuwa mradi huo utakamilika kwa wakati na kuwanufaisha wananchi wote.

“Nimeona changamoto nyingi katika usambazaji wa maji kwa maeneo ya mjini. Kuna maeneo mengi ambayo hayapati maji kwa wakati. Nimemuagiza Meneja wa mamlaka ya maji mjini Tunduru (TUUWASA)  kushughulikia changamoto zote pamoja na kuzitafutia ufumbuzi. Pia, anapaswa kuandika ripoti juu ya changamoto hizo haraka iwezekanavyo,” alisema Mhe.Eng. Mahundi.

Ziara hiyo ya Mhe.Eng. Mahundi ni mwendelezo wa ziara zake za kukagua miradi ya maji katika maeneo mbalimbali nchini. aliahidi kwamba Serikali itaendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma bora ya maji.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.