• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

ZIARA ya Naibu Katibu Mkuu, Elimu ( OR TAMISEMI) Tunduru.

Imewekwa : November 21st, 2023

Naibu Katibu Mkuu, Elimu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ,Dkt. Charles Msonde, amefanya ziara ya kikazi wilayani Tunduru, Mkoani Ruvuma, kukagua miradi ya maendeleo sekta ya Elimu.

Katika ziara hiyo, Dkt. Msonde alionyesha kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa miradi hiyo ambayo ipo katika hatua ya umaliziaji. Alisema kuwa miradi hiyo itasaidia kuboresha upatikanaji wa elimu bora kwa wanafunzi wa wilaya ya Tunduru. Pia, ametoa maagizo kwa viongozi wa shule hizo na kamati zinazosimamia miradi hiyo, kuhakikisha kuwa miradi hiyo inakamilishwa kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Dkt. Msonde alikagua ujenzi wa shule mpya iliyopo katika kata Tuwemacho, mradi uliogharimu zaidi ya shilingi milioni 560, Mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 30 mwezi Novemba mwaka huu. Pia, alikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa, mabweni na matundu ya choo katika shule za sekondari Masonya, Tunduru na Nandembo.

Alisema kuwa Serikali inaendelea kuwekeza katika sekta ya Elimu ili kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata elimu bora na yenye ubora. Alisisitiza kuwa suala la ujenzi uaminifu na uadilifu, mahitaji ya miundombinu ni mengi lakini wataalamu na wasimamizi wote wanapaswa kusimamia kikamilifu kuhakikisha miradi yote inakamilika.

“Miradi hii ikikamilika kwa wakati na ubora itasaidia kupunguza umbali kwa watoto wetu waliokuwa wakilazimika kutembea kwa muda mrefu kwenda mahali shule ilipo, Maendeleo yanaanzia kwenye Elimu” Alisema Dkt. Msonde “Lengo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha anaboresha miundombinu yote ya Elimu ili watoto wapate elimu karibu na katika mazingira bora”.

Baada ya kukagua miradi hiyo, Dkt. Msonde aliridhika na utekelezaji wake, aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kutoa fedha za miradi ya maendeleo, na pia aliwapongeza wabunge wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Daimu Mpakate (Jimbo la Tunduru Kusini) na Mh. Hassan Kungu (Jimbo la Tunduru Kaskazini) pamoja na madiwani wote, kwa kuendelea kutekeleza ilani ya Chama cha mapinduzi. Vilevile, alimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru Ndg. Chiza C. Marando pamoja na timu yake ya wataalamu na kamati za ujenzi kwa kusimamia vyema utekelezaji wa miradi hiyo.

Ukaguzi huu wa miradi wa mara kwa mara unasaidia kutambua mapungufu yoyote katika utekelezaji wa miradi, na hatua za kurekebisha mapungufu hayo huchukuliwa mara moja. Ukaguzi huangalia utekelezaji wa miradi ya maendeleo hiyo kwa kuzingatia mambo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na uwiano wa gharama na kazi iliyofanyika, ubora wa vifaa na kazi zilizofanywa, muda wa utekelezaji wa mradi na matumizi sahihi ya fedha za mradi.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.