• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

ZAIDI ya milioni 200 kukamilisha kituo cha Afya Juma Homera.

Imewekwa : November 3rd, 2023

Mkuu wa wilaya ya Tunduru, Mheshimiwa, Wakili Julius S. Mtatiro amekagua maendeleo ya ujenzi na ukarabati wa kituo cha Afya Juma Homera, kilichopo kata ya Nakayaya wilayani humo.

Kituo hicho cha afya kilianza kujengwa chini ya usimamizi wa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mheshimiwa Juma Homera, ambaye kwa sasa ni mkuu wa mkoa wa Mbeya. Mh. Homera alikutana na wadau mbalimbali ambao walichangia na kuunda kamati za usimamizi ili kuanzisha ujenzi wa kituo hicho.

Ujenzi na ukarabati wa mradi huo unagharimu zaidi ya shilingi milioni 200, fedha ambazo zimetokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Tunduru, ambao unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Januari mwaka 2024.

Mh. Wakili Mtatiro aagiza kampuni ya usambazaji wa umeme (TANESCO) kuhakikisha wanarejesha Transfoma waliyoiondoa maeneo ambayo mradi huo wa ujenzi na ukarabati unaendelea.

“Ninafahamu kwamba TANESCO Tunduru walikumbana na changamoto mbalimbali ndio maana wakaondoa Transfoma iliyokuwa maeneo haya ambayo Mradi wa kituo chetu cha afya unaendelea” Alisema Mh. Mtatiro, “Namwagiza Meneja wa TANESCO Tunduru atafute mbadala wa Transfoma hiyo ili kusaidia mradi huu kukamilika kwa muda uliopangwa”

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Daktari Renatus Mathias, ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kuiwezesha Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, vilevile amemshukuru Mbunge wa Tunduru Kaskazini Mh. Hassan Zidadu Kungu pamoja na waheshimiwa madiwani wote.

Ujenzi na ukarabati wa kituo cha afya Juma Homera upo katika hatua ya umaliziaji, ujenzi wa kituo hicho ni moja kati ya mikakati ya serikali ya awamu ya sita chini ya Raisi wake Mheshimiwa, Daktari, Samia Suluhu Hassan, katika kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma za afya zilizo bora.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.