• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

ZAIDI ya bilioni 12 zaingia katika mpango wa kunusuru kaya masikini Tunduru

Imewekwa : March 12th, 2024

Kwa kipindi cha miaka mitatu Halmashauri ya wilaya ya Tunduru imepokea Zaidi ya bilioni 12 kwa ajili ya ruzuku ya walengwa pamoja na usimamizi ngazi ya wilaya.  

Mratibu wa TASAF (W), Bwn.Muhidin Shaibu ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuonesha nia ya dhati katika kupambana na umaskini katika Wilaya ya Tunduru, ambapo Mpango huu wa kunusuru kaya maskini umejikita katika uhawilishaji wa ruzuku kwa walengwa, Miradi ya ajira za muda (PWP), Ruzuku ya uzalishaji, na Ujenzi wa miradi ya miundombinu.

“Halmashauri ya wilaya ya Tunduru ina jumla ya kaya 20,228 kutoka katika vijiji 157 vilivyopo wilayani, Katika kipindi cha miaka mitatu ya awamu ya sita, tumefanya malipo kwa awamu kumi na tano” Alisema Bwn. Muhidin “Halmashauri ya wilaya ya Tunduru ni miongoni mwa wilaya zinazolipa malipo kwa njia ya mtandao (e-payment) na Jumla ya kaya 4,341 zimepokea kwa njia ya Benki na kwa njia ya mtandao wa simu na kaya 15,887 zilipokea kwa mfumo wa fedha taslimu (cash)”

Vile vile, Halmashauri inatekeleza aina mbalimbali ya miradi ambayo ni uboreshaji visima vya asili, ujenzi wa barabara za jamii, mashamba ya miti na matunda, ujenzi wa vivuko na uchimbaji wa mabwawa ya kuhifadhi maji. Takwimu za miradi hii ni kama ifuatavyo, mikorosho idadi 36,257 katika eneo la ekari 323.7 imepandwa, miti ya mbao mitiki 36,790, ujenzi wa barabara za jamii km 1311, miti ya matunda miembe 560 eneo la ekari 14 na kuboresha visima 15 vya asili.

Kaya zote zilizoandikishwa kwenye Mpango ambazo hazina nguvu kazi zitapata ruzuku ya msingi,ruzuku ya kutimiza masharti ya elimu na afya. Kadhalika kaya zitapata fursa ya kuongeza kipato kwa kushiriki katika kazi za ajira ya muda.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya za Walengwa nchini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF). Lengo kuu la Mpango huu ni kuziwezesha kaya maskini zaidi kuweza kuongeza matumizi ili kumudu kugharamia mahitaji muhimu ya kaya.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.