• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Wazazi Timiseni Wajibu wenu kwa Watoto

Imewekwa : May 3rd, 2019

Na theresia mallya Tunduru.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mhe.Juma Zuberi Homera wakati akizindua zoezi la ugawaji wa dawa za kingatiba kwa magonjwa yalikuwa hayapewi kipaumbele ngazi ya shule Wilaya iliyofanyika katika shule ya msingi Muungano.

Akisoma taarifa kwa mgeni rasmi mratibu wa chanjo wilaya kwa niaba ya Mganga mkuu wilaya Dkt.Wendy Robert alisema magonjwa yasiyopewa kipaumbele ni pamoja na Kichocho, Minyoo ya Tumbo,Trachoma, Usubi, Mabusha na Matende, aliyataja magonjwa ambayo  kingatiba hutolewa ngazi ya shule kuwa ni Kichocho na Minyooo ya tumbo.

Aidha alisema katika kipindi  cha mwaka 2019 Halmashauri kupitia Idara ya afya kwa kushirikiana na Idara ya Elimu msingi wanatarajia kutoa chanjo kwa wanafunzi wapatao 71309 ikiwa wasichana 35288 na wavulana 36021 kutoka katika shule 150 za msingi wilayani Tunduru.

Mratibu wa chanjo alisema "Mwaka 2018 tulitarajia kutoa kingatiba kwa wanafunzi wapatao 67364 lakini wanafunzi waliokunywa dawa ni 65815 ikiwa Wasichana 32663 na wavulana 33152 sawa na asilimia 98 ya malengo tuliyotarajia kuyafikia ya asimilia 100 kwa wanafunzi wote wa shule za msingi wilayani Tunduru"

 Magonjwa haya ya kichocho na minyoo ya tumbo huambikizwa kwa njia ya maji kwa binadamu mwenye vijimelea kutotumia choo hivoo vimelea kusambaa au kuchangamana na maji na huenea kwa binadamu kugusa maji hayo,huku minyoo ya tumbuo ikienezwa kwa u;aji wa vyakula visivyopikwa vizuri ama matunda yasiyooshwa vizuri, kutovaa viatu, kula bila ya kunawa mikono.

Katika picha ni wanafunzi wa shule ya msingi Muungano wilayani Tunduru wakiwa katika picha ya Pamoja wakati wa uzinduzi wa chanjo kinga dhidi ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele,ambapo jumla ya wanafunzi 71309 katika shule 150 wanatarajiwa kumeza dawa hizo kuanzia mei 03 2019.

Mratibu alisema kuwa madhara yatokanayo na magonjwa  haya yasipotibiwa  kichocho husababisha kutoka kwa damu kwenye mkojo na kinyesi,saratani ya tumbo, kibofu cha mkojo na ini.

Minyoo ya tumbo husababisha watoto kuwa dhaifu, kuishiwa damu, utumbo kujifunga na kifafa, mahudhurio hafifu na mandeleo duni shuleni.

Naye mkuu wa wilaya ya Tunduru Mhe.Juma Zuberi Homera alianza kwa kuwapongeza walimu wa shule ya msingi muungano kwa usimamizi bora katika taalum, pia Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kupitia idara ya afya kitengo cha uratibu wa chanjo kwa kufanya kazi ya usambazaji wa chanjo katika vijiji mbalimbali vya wilaya ya Tunduru.

Juma Homera aliwataka wazazi na walimu wote wenye watoto katika shule za msingi 150 wilaya ya Tunduru kuhakikisha watoto wote wanapata dawa za kinga dhidi ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele ili kuendandana na kauli mbiu ya ‘Tunduru  bila magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele sasa inawezekana, timiza wajibu kwa kumeza dawa, kingatiba, ishi kwa furaha’

Watoto wapewe haki zao za msingi ikiwa pamoja na watoto kupewa haki ya kupata elimu katika mazingira rafiki kama upatikanaji wa chakula shuleni,hivyo niwaagize wazazi wote wa wilaya ya Tunduru tuwachangie watoto wetu chakula shuleni ili waweze kusoma vizuri na kutengeneza taifa lenye tija.

Nimalizie kwakuwaomba wazazi wote wilaya ya Tunduru kuhakikisha kwamba watoto wotewanakunywa dawa hizi ndani ya Wilaya ya Tunduru kwani hazina madhara yoyote kwaafya ila ni kinga dhidi ya magonjwa ya Kichocho,Trachoma,Minyoo ya tumbo, Mabusha,Usubina Matende.

Mwisho.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.