• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi Watakiwa Kufanya Kazi kwa Weledi

Imewekwa : October 3rd, 2019

Theresia Mallya          03.10.2019

Katika kuhakikisha kuwa kanuni taratibu na miongozo inafuatwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba 24, 2019 wasimamizi wasaidizi katika vituo wanatakiwa kusoma, kuelewa na kufuata miongozo na ratiba ya uchaguzi huo.

Hayo yamesemwa na katibu tawala Mkoa wa Ruvuma Profesa Riziki Shemdoe katika ufunguzi wa semina kwa wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata na Vijiji katika vituo vyote vya uchaguzi wa serikali za mitaa.

Akisoma taarifa ya maandalizi yaliyofanywa na Halmahauri ya wilaya ya Tunduru Kaimu Afisa uchaguzi Ndg Abdul Kasembe amesema kuwa msimamizi wa uchaguzi amekua akifuata ratiba ya uchaguzi kama ilivyo katika mwongozo wa uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2019, aidha  Halmashauri  ina jumla ya vituo vya uchaguzi wa serikali za mitaa 1179 ambavyo vitatumika katika uchaguzi huo.

Akiongea na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ambao pia watendaji wa Kata na Vijiji  wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya wawezeshaji kwa waandikishaji wa orodha ya wapiga  kura, Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Profesa Riziki Shemdoe ambaye pia ni Msimamizi mkuu wa Uchaguzi mkoa alianza kwa kuwapongeza watendaji wote kwa kazi nzuri wanayofanya ya usimamizi hasa katika eneo la ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri.

Msimamizi wa uchaguzi Halmashauri ya wilaya ya Tunduru mwalimu Anderson Mwalongo akitoa maekelezo kwa wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa katika mafunzo kwa uwezeshaji kwa waandikishaji wa orodha ya wapiga kura.

Prefesa amesema “niwapongezeni kwa usimamizi mzuri wa mapato kufikia 59% ya makusanyo ya ndani licha ya 51% ya makusanyo yaliyokuwa yameelekezwa kwenye ushuru wa zao la korosho kutokuwepo, hongereni sana” lakini pia mnapaswa kuendelea kusimamia mapato , kuwa waaminifu, na kufanya kazi kwa uadilifu na kuzingatia Sheria,Taratibu na Kanuni za utumishi wa Umma.

Pia niwatake muendelee kutoa ushirikiano katika kutekeleza majukumu, lakini pia niwaombee muendelee kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali katika maeneo yenu ya utawala ili kuleta tija kwa wananchi mnaowasimamia.

Vilevile Profesa Shemdoe aliwataka wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa kufanya maamuzi sahihi katika kila hatua wanayochukua katika masuala yote ya uchaguzi wa serikali za mitaa.

Katika picha ni wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya Kata na Vijiji  wakipewa mafunzo elekezi ya namna ya kusimamia shughuli za uchagauzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 24, 2019.

Profesa Shemdoe ameendelea kusisitiza wasimamizi kuhakikisha kwamba wanasoma  kanuni na mwongozo wa serikali za mitaa, kuzielewa kujua nini kifanyike na kufuatwa katika taratibu za uchaguzi, pia mzingatie ratiba ya uchaguzi wa serikali za mitaa inaelekeza nini.

Wasimamizi wasaidizi mnatakiwa kuwepo katika vituo vyenu vya kazi muda wote wa uchaguzi ili kuondoa mikanganyiko ambayo inaweza kujitokeza wakati wote wa maandalizi hadi kufanyika kwa uchaguzi novemba 24, aidha kwa wasimamizi wa uchaguzi wasaidizi hakutakuwepo na ruhusa au likizo mpaka uchaguzi utakapokwisha na kutowepo doasari katika eneo lako la uchaguzi.

Hata hivyo alimalizia kwa kuwapongeza Mkurugenzi Mtendaji halmashauri Ndg Gasper Balyomi pamoja na msimamizi wa uchaguzi Halmashauri ya Tunduru Mwalimu Anderson Mwalongo  kufanya maandalizi vyema na kufuata ratiba iliyopo katika mwongozo wa uchaguzi wa serikali za mitaa kwa mwaka 2019.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.