• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Waratibu Elimu Kata Vaeni viatu Vyenu.

Imewekwa : May 3rd, 2018

“Naomba unapokwenda kuitembelea shule usikubali kwenda kama hujui unakwenda kufanya nini”hayo yalisemwa na Afisa Elimu wilaya mwalimu Anderson Mwalongo alipokutana na maafisa elimu kata katika ukumbi wa klasta kujadili utekelezaji wa maagizo ya afisa elimu mkoa juu ya mikakati ya kuboresha sekta  elimu wilayani Tunduru.

Mwalimu Mwalongo alisema ili kuboresha kiwango cha ufaulu katika halmashauri ya wilaya ya Tunduru ni lazima maafisa elimu kata kufanya kazi kwa weledi na kurudisha nidhamu ya mwalimu katika shule zilizopo katika kata wanazosimamia.

Pia alitoa maelekezo ya namna bora ya kufaya usimamizi wa shule za msingi na sekondari zilizopo katika kata zao ili kuhakikisha kuwa walimu wanafundisha kulingana na sera ya elimu ya mwaka 2003, kuwa na maandalio, na kutoa mitihani ya kila wiki na mwezi ili kuwapima wanafunzi.

Mwalimu Mwalongo aliendelea kutanabaisha kuwa Maafisa Elimu Kata wanatakiwa kuwa na mpango kazi (work Plan) wenye chachu au tamaa ya kufikia lengo fulani katika shule zote zilizopo ndani ya Kata husika, kufanya kazi zenye matokeo chanya wakati wa  kutekeleza sera na miongozo mbalimbali ya elimu inayotolewa na serikali na kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu iliyo bora na sio bora elimu.

Maafisa Elimu Kata kutoka wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru wakifuatilia kwa karibu maagizo ya Ofisa Elimu wilaya Mwalimu Anderson Mwalongo ambaye hayupo katika picha katika kikao cha kazi kilichofanyika ukumbu wa klasta ya Mlingoti mapema leo hii, kwa ajili ya kuwakumbusha namna bora ya utendaji kazi katika kusimamia elimu wilayani Tunduru.

Aliendelea kwa kuwataka Maafisa  hao kufanya kazi na kuepuka siasa na kufanya kazi zao kwa kuzingatia lengo alilojiwekea, “unapoenda kufanya usimamizi kwenye shule epuka maneno mengi, wewe sio mwanasiasa nenda kwenye lengo lako mara moja na pia muwe na tabia ya kuweka kumbukumbu ya ushauri na maagizo mnayotoa kwa wakuu wa shule mara mtembeleapo shule kuona maendeleo ya taaluma kwa wanafunzi” alisema Ofisa Elimu Msingi.

Pia aliwataka waratibu/maafisa elimu kata kuvaa viatu vyao pale mkuu wa shule anapokiuka maadili ya kazi ya ualimu, kanuni na taratibu za uendeshaji mzima wa sekta ya elimu katika shule yake kuweza kuwachukulia hatua za kidhamu, ikiwa ni pamoja na kutoa ushauri, barua za onyo na hata kumuwajibisha pale anaposhindwa kutekeleza majukumu yake, kwa kufanya hivi kiwango cha ufaulu kitaongezeka.

Hata hivyo mwalimu Anderson Mwalongo alimalizia kwa kuwataka Maafisa Elimu Kata kuhakikisha KASIKI za kuhifadhia mitihani zinajengwa katika kila shule ya msingi iliyopo katika Kata anazosimamia, na kwa shule ambayo hawatajenga kasiki hizo mpaka kipindi cha mitihani, mkuu wa shule atapata gharama ya kusafirisha mitihani hiyo kwa shule jirani ambayo wana kasiki ya kutunza mitihani.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.