• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WANANCHI TUNDURU WAPATIWA MAFUNZO YA UHIFADHI RASILIMALI NA MALIASILI.

Imewekwa : June 10th, 2023

Umefanyika muendelezo wa mafunzo ya uhifadhi rasilimali asili yaliyotolewa katika wilaya ya Tunduru kupitia uwezeshaji wa muungano wa mashirika ya uhifadhi wa rasilimali na maliasili .kwa Wilaya ya Tunduru ,shirika moja wapo la  utoaji mafunzo hayo la Honeyguide limetoa mafunzo  hayo kupitia mradi wa Kujenga Usimamizi Wa Asili (KUWA) wenye dhima kuu ya kujenga uwezo katika utawala wa kusimamia rasilimali na maliasili kwa usawa ili kutengeneza njia za kuboresha maisha na kuzalisha manufaa endelevu ya kiuchumi,kimazingira na kijamii.

Mafunzo hayo yalihudhuriwa na jumuiya mbili za uhifadhi wanyama pori za wilaya ya Tunduru ambazo ni NALIKA na CHINGOLI  ambapo walipatiwa elimu juu ya utawala bora na jamii endelevu  zenye mahusiano  chanya na uhifadhi wa rasilimali na maliasili na mazingira kwa ujumla.

Afisa mjenga uwezo wa shirika la Honeyguide ndg.Prosper Frank Munisi amewataka wananchi wa jumuiya hizo za uhifadhi  kuwa na usimamizi endelevu wa rasilimali zetu ,mafunzo haya waliopata wanajumuiya ya uhifadhi wa rasilimali yatawasaidia katika kuwa na uwezo wa kusimamia  rasilimali hasa katika misingi mitatu ya uendelevu wa kijamii,uendelevu wa kiuchumi na uendelevu wa kimazingira kwa usawa.

Pia alisema anawaomba wanajumuiya za uhifadhi kushirikiana katika kutatua changamoto zinazokumba uhifadhi wa rasilimali na maliasili katika meneo yetu tunayotoka.

Mfunzo hayo yalihudhuriwa pia na mwenyekiti wa jumuiya ya NALIKA  wilaya ya Tunduru pia ni mwenyekiti wa muungano wa jumuiya za uhifadhi Tanzania ,Ndg.Saidi Rashidi Masoud , kwa upande wake aliwataka wanajumuiya wote ,elimu hiyo waliopata waweze kuinenza kwa wananchi wa maeneo waliotoka ili nao waweze kuwa na elimu juu ya uhifadhi wa rasilimali za asili  na kuweza kupunguza uvamizi na ujangili ambavyo ni vitendo vitakavyoweza kupoteza maliasili na rasilimali zetu.

Tunaushukuru muungano wa mashirika ya uhifadhi wa rasilimali na maliasili hasa Honeyguide kwa mafunzo haya  tuliyoyapata tunahaidi  kuyatendea kazi yale yote tuliyoyapata kwa manufaa ya uhifadhi wa mazingira na maliasili  alisema miss Jamila Abdallah, askari uhifadhi wanyamapori (VGS) kijiji cha  twendembele.



Baadhi ya wanajumuiya za uhifadhi wa rasilimali na maliasili wilaya ya Tunduru wakiwa katika kundi la majidiliano,wakijadili kuhusu visababishi vya uharibifu wa maliasili na rasilimali asili katika maeneo yetu.wanajuiya wakiwa katika darasa kujifunza kuhusiana na utawala bora na jamii endelevu katika kuhifadhi rasilimali na mali asili ili kuleta tija katika misingi ya kiuchumi, kijamii na kimazingira.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.