• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Wakulima Tumieni fedha vizuri kuboresha Elimu na Afya

Imewekwa : November 22nd, 2019


Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma Mhe. Julius Mtatiro amewataka wakulima wa zao la korosho kutumia vizuri fedha wanazopata katika kuwapeleka watoto shule na kukata bima ya afya ya jamii iliyoboreshwa ili kusaidia familia katika kuleta maendeleo wilayani Tunduru.

Ameyasema hayo katika mnada wa tatu wa Korosho uliofanyika katika kijiji cha majimaji tarehe 21 Novemba 2019 ambapo kampuni mbili za Alfa Choice na Sunshine zilishinda zabuni hiyo kati ya wanunuzi 34 waliojitokeza katika mnada huo ambapo jumla ya  kilo 2,979,407 zilinunuliwa kwa  bei ya wastani ya shilingi 2773.19 kwa kilo.

Mwenyekiti wa Chama kikuu cha ushirika wilayani Tunduru Ndg.Hashimu Mbalabala akitoa matokeo ya Mnada wa tatu kwa wananchi wa Majimaji waliojitokeza kushuhudia mnada huo kwa niaba ya wananchi wa wilaya ya Tunduru ambapo wanunuzi walikua 34 lakini waliotenda kwa bei ya juu na kununua korosho zilizokua mnadani ni Kampuni ya Sunshine na Alfa choice kwa bei ya shilingi 2773.19 kwa kilo.

Aidha Mhe.Mtatiro amewapongeza wanunuzi walioshinda zabuni hiyo na kuwataka wanunuzi wanaotenda kwa bei ya chini kuwa hawatapata Korosho za wilaya ya Tunduru hivyo wajipange.

Pia mkuu huyo wa wilaya ametoa maagizo kwa mkuu wa jeshi la polisi wilayani Tunduru kuhakikisha kuwa wanashughulikia malalamiko ya wanunuzi wa korosho ya kukumbana na vipingamizi  barabarani wanapowahi katika minada ya kununua korosho Tunduru. “OCD fanya mawasiliano na wenzio wa wilaya jirani ili kuondoa usumbufu kwa wanunuzi wanapawahi kwenye mnada Tunduru” alisema Julius Mtatiro.

Vile vile aliwata mweneyekiti wa chama kikuu cha Ushirika pamoja na Meneja wa Chama hicho kuhakikisha kuwa magunia kwa ajili ya kufungashia korosho za wakulima yanafika kwa wakati wilayani Tunduru ili kuhakikisha korosho zilizopo katika maghala ya vijiji zinasasfirishwa kwenye ghala kuu kabla ya msimu wa mvua kuanza.

Afisa Ushirika Wilaya Ndg.George Bisani akisoma barua za zabuni za wanunuzi wa zao la Korosho katika mnada wa tatu uliofanyika katika Kata ya Majimaji.

Hata hivyo alimalizia hotuba yake kwa kuwaagiza viongozi wa bodi ya korosho kuandaa mkutano na vyama vyote vya msingi wilayani Tunduru ili kuondoa sintofahamu inayoendelea kwa baadhi ya vyama na waandhishi wanaowaibia wananchi, na wananchi kutoa taarifa za watu wanaojihusisha na ununuzi haramu wa korosho (Kangomba) ili serikali iwachukulie hatua kwani kufanya hivyo ni kumkandamiza mkulima.


Theresia Mallya

Tunduru                                                                                        

 22/11/2019

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.