• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Waandishi Elimisheni wazazi Umuhimu wa kusoma na watoto

Imewekwa : December 7th, 2018

"Waandishi wa Habari  watakiwa kuwa wakala wa  mabadiliko katika kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa wazazi kusimamia watoto kujua K tatu" hayo yamesemwa na Katibu Tawala mkoa wa Ruvuma  Profesa Riziki Shemdoe katika kikao kazi cha mrejesho wa simulizi za mabadiliko kilichofanyika katika ukumbi wa Jimbo Mbinga.

Akitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa siku mbili kwa  washiriki kutoka katika Halmashauri nane za mkoa wa Ruvuma na waandishi wa habari,  Afisa mipngo mkoa ndg Edmund Siame  alisema lengo la mrejesho wa simulizi za mabadiliko ni kubadilishana na kujifunza mbinu  walizotumia kufanikiwa katika kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya elimu mkoani kupitia  mpango  wa Tusome pamoja.

washiriki wa Tusome Pamoja wakimsikiliza katibu Tawala Mkoa Profesa Riziki Shemdoe wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mrejesho wa Simulizi za mabadiliko kutoka katika Halmashauri zote nane za mkoa wa Ruvuma.

Alisema ili kuleta uhalisia na kutoa mrejesho chanya kwa wafadhili wa huu wa Tusome Pamoja ni Halmashauri zote kutoa  simulizi zenye  uhalisia kwa kuzingatia chazo tatizo, ukubwa, takwimu halisi zinazohusiana na tatizo hilo na suluhisho.

"natoa agizo kwa Afisa Habari Ofisi ya mkuu wa mkoa kushirikiana kwa karibu na maafisa walioko katika Halmashauri zote nane kuwajengea uwezo wa kuandaa makala za simulizi za mabadiliko kuonesha ufanisi wa kazi zinazofanywa katika Halmashauri zao na mkoa wa Ruvuma kwa ujumla"

Afisa Mipango Ndg. Edmund Siame alisema kuwa ili kutokomeza tatizo la wanafunzi wasiojua kusoma, kuandika na kuesabu katika mkoa wa Ruvuma linaweza kuisha kwa kushirikiana vizuri na waandishi wa habari kwani ni wakala wa amabadiliko katika jamii wakitumiwa vizuri. 

Mratibu wa Mpango wa Tusome Pamoja mkoa wa Ruvuma ndg Stephen Msabaha akiongea na washiriki kutoka halmashauri nane za mkoa wa Ruvuma  (ambao hawako kwenye picha) wakati wa Ufunguzi wa mkutano siku mbili wa kutoa mrejesho wa maandalizi ya Simulizi za Mabadiliko

"niwaombe waandishi wa habari kutoa na kutengeneza vipindi vya kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa elimu kwa wazazi pamoja na walezi kusoma na watoto wao jioni wanaporudi nyumbani lakini pia kuwa na tabia ya kufuatilia na kukagua madaftari ya watoto ili kujenga ueuelewa,ajua vyombo vya habari vina nguvu kubwa ya kuleta mabadiliko " alisema Kaimu katibu Tawala mkoa ndugu Edmund Siame

vilevile alisema mpango wa Tusome Pamoja wamefanya kazi kubwa toka umeanza ikiwa ni utoaji wa vitabu vya kusoma darasa la kwanza na pili, kuboresha madarasa na matundu ya vyoo pamoja na mazingira ya kufundishia na kujifunzia.

Muwezeshaji wa Mpango wa Tusome Pamoja Taifa Ndg Furaha Kabuye akitoa maoni ya maboresho ya Simulizi za Mabadiliko zilizokuwa zinatolewa na washiriki kutoka Halmashauri nane za mkoa wa Ruvuma.

"Mapitio yafanyike kwa wanafunzi wa darasa la pili wanaoingia darasa la tatu wasijua Kusoma, Kuandika na Kuhesabu wachujwe na kurudishwa darasa la pili ili kumaliza kabisa tatizo KKK katika wa Ruvuma ifikapo 2020 , na niwaagize Maafisa Elimu wote kufanya mapitio ya wanafunzi waliopo sekondari wasiojua KKK kuondolewa mara moja"

Hata hivyo aliwapongeza washiriki kwa kazi kubwa waliofanya kwani inatia moyo kuona kuna mabadiliko chanya yanayochangiwa na Kamati za shule, wahamasishaji Elimu Jamii (WJE), Umoja wa wazazi na walimu (UWAWA), wadau mbalimbali wa Elimu na Halmashauri zote kutoa ushirikiano mkubwa kuchangia mpango wa Tusome Pamoja katika kuboresha Miundombinu ya madarasa, Upatikanaji wa chakula shuleni na kupunguza wanafunzi wasiojua Kusoma, Kuandika na Kuhesabu.



Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.