• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

UDAHILI KIDATO CHA KWANZA WAPAA TUNDURU.

Imewekwa : February 8th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mhe. Adv, Julius S. Mtatiro, amehitimisha vikao vya kazi vya kufuatilia udahili wa kidato cha kwanza mwaka 2024

Akizungumza katika vikao kazi na Watendaji wa Kata,waratibu Elimu kata, Wakuu wa shule na watendaji wa vijiji, amewapongeza kwa juhudi zao za kuhakikisha wanafunzi wote wanapata nafasi za kuendelea na masomo yao ya Sekondari.

Ambapo mpaka kufikia Februari 05, 2024 asilimia 86 ya Wanafunzi wa kidato cha kwanza wamedahiliwa shule za sekondari na kufanya Takwimu kwa kila Tarafa kuwa, Tarafa ya Nakapanya asilimia 96.4, Tarafa ya Mlingoti asilimia 95.6, Tarafa ya Namasakata asilimia 88.4, Tarafa ya Nampungu asilimia 85.8, Tarafa ya Matemanga asilimia 81.1, Tarafa ya Lukumbule asilimia 79.4,  na Tarafa ya Nalasi asilimia 78.7.

Mhe. Mtatiro amesema kuwa, amefurahishwa na kasi ya udahili katika kata nyingi, na amewataka Watendaji kuendelea na juhudi zao ili kuhakikisha asilimia 100 ya wanafunzi waliohitimu darasa la saba wanadahiliwa kidato cha kwanza,pia Mh. Mtatiro ameahidi kutoa ushirikiano wake kwa Watendaji wote katika kuhakikisha udahili unakamilika kwa mafanikio.

"Nimefurahishwa  na maendeleo ya udahili katika wilaya yetu. Hii ni ishara ya juhudi kubwa zinazofanywa na Watendaji wetu katika kuhakikisha Watoto wote wanapata Elimu bora." Alisema Mhe. Mtatiro

Aidha, amewataka Watendaji kuunda mikakati ya ndani ili kuendelea  kuhamasisha Wazazi na walezi kuwapeleka Watoto wao shule, na pia kutafuta suluhu kwa changamoto zinazokwamisha udahili. Baadhi ya changamoto zilizotajwa ni pamoja  na baadhi ya Wanafunzi kutoka familia zenye mahitaji maalum, hasa wale wanaolelewa na bibi na babu waliozeeka sana baada ya wazazi kuwatelekeza, hawajapata nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza. Baadhi ya wazazi kukimbilia mashambani na misituni kujificha ili wasipeleke watoto wao sekondari.

Kwa upande wao Watendaji wa Kata pamoja na vijiji wamehaidi kushirikiana na serikali ya Wilaya kuhakikisha asilimia ya Wanafunzi ambao bado hawajadahiliwa wataweza kudahiliwa  kabla ya kufungwa kwa dirisha la udahili wa wanafunzi kidato cha kwanza.

Vikao kazi vilivyofanyika na Mkuu wa Wilaya vimetoa msukumo mkubwa kwa Watendaji wa kata katika kuhakikisha udahili wa kidato cha kwanza unakamilika kwa mafanikio. Kwa ushirikiano wa pamoja kati ya serikali na wananchi, wilaya ya Tunduru ina lengo la kufikia asilimia 100 ya udahili katika mwaka huu wa masomo.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.