• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

UCHAGUZI VYAMA VYA USHIRIKA TUNDURU.

Imewekwa : February 29th, 2024

Ofisi ya Usimamizi Maendeleo ya Ushirika Wilaya ya Tunduru imefungua Mikutano Mikuu ya kawaida ya vyama vya Msingi vya  ushirika. Mikutano hii inajumuisha uchaguzi wa bodi mpya za vyama hivyo.

Ufunguzi huo ulifanyika katika Chama cha Msingi cha Ushirika Mtetesi (Mtetesi AMCOS) katika kata ya Mindu. Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi wa vyama vya ushirika, wanachama, na Viongozi kutoka ngazi mbalimbali za Serikali.

Katika mkutano huo, uchaguzi ulifanyika kuchagua bodi mpya ya kusimamia na kuongoza Chama cha Msingi cha Ushirika Mtetesi. Uchaguzi huo ulifanyika kwa mujibu wa utaratibu uliotolewa na Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC), unaotaka vyama vyote vya ushirika kuendesha uchaguzi wa uongozi wa bodi mwaka huu 2024.

Akizungumza baada ya uchaguzi huo, Afisa Ushirika (W) Tunduru Ndg. George N. Bisani aliipongeza bodi mpya iliyochaguliwa ya Chama cha Msingi cha Ushirika Mtetesi. Aliisisitiza bodi hiyo kutengeneza mikakati ya ndani ya chama ili kuweza kukiinua kiuchumi zaidi ya pale kilipo sasa.

Bw. Bisani pia aliitaka bodi mpya kuhakikisha Wanachama na Wakulima wanasajiliwa katika Mfumo Mpya wa Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (MUVU).

"Tugombane kuhusu maendeleo, ili tuzidi kuwaita wawekezaji katika chama chetu," alisema Bw. Bisani. "Kinachomvutia Mkulima kujiunga uanachama ni uadilifu wa uongozi."

Kwa upande wake, Mwenyekiti aliechaguliwa wa Bodi ya Chama cha Msingi cha Ushirika Mtetesi Bw. Adamu Rashidi Mpelela ameahidi kuonesha ushirikiano wa moja kwa moja kwa bodi iliyochaguliwa pamoja na wanachama ili kuweza kuinua chama kiuchumi.

"Sisi tumechaguliwa kutoka miongoni mwenu wanachama tunaomba ushirikiano wenu wa dhati katika kufikia mafanikio ya chama," alisema Bw. Mpelela.

Sambamba na hayo, Diwani wa Kata ya Mindu, Mhe. Richard Bazil Nakoko, ameisisitiza bodi iliyochaguliwa kubadili mwenendo wa chama ili kuweza kupata mafanikio, hasa katika uchumi wa chama hicho.

Mkutano huo ulihitimishwa kwa wito kwa viongozi wapya wa vyama vya ushirika kushirikiana na wanachama wao ili kuleta maendeleo ya vyama vyao na kuinua maisha ya wananchi.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.