• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Bi Bumi atoa cheti kwa Mnatinga Amcos

Imewekwa : February 2nd, 2019

Akisoma taarifa ya Chama cha Ushirika  Mnatinga katibu wa chama  Ndg Mohamed Abdalah Arobaini alisema  chama kina jumla ya wanachama wapatao 98 kutoka  katika Kata nane  za Namakambale, Ngapa, Tinginya, Mindu,  Nakapanya, Mchuluka, Mtina na Chiwana.

Aliendelea kusema kuwa Amcos  ya Mnatinga ina lengo la kuongeza  idadi ya wanachama hadi kufikia 426 toka 98 wana sasa lakini  chama kitakua  kinafanya kazi ya kununua  mazao Mchanganyiko na pia kutoka wigo wa kuanzisha kiwanda cha kukamua mafuta ya Ufuta na Alzeti ilimradi kukuza uchumi wa  wananchi.

Akizungumza na wanachama wa  Amcos ya Mnatinga Mrajisi Msaidizi mkoa wa Ruvuma Bi Bumi Masuba alianza kwa kuwapongeza wanachama kufanikiwa kufikia malengo ya kuanzisha chombo ambacho kitawasaidia kupata nguvu ya kujiendeleza kwa mwananchama  mmojammoja  ili kutelekeza kauli mbiu ya ushirika tujenge uchumi wenye nguvu.

Katibu  wa Amcos ya Mnatinga akisoma taarifa ya Chama  hicho  kwa wanachama na Mrajisi  Msaidizi  mkoa wa Ruvuma Bi Bumi  Masuba katika mkutano maalum wa uchaguzi na kukabidhi cheti ulifanyika mapema wiki hii shule ya msingi Songambele wilayani Tunduru.

 Bi Bumi Masuba  alisema kuwa Mnatinga iki kufikia malengo waliyojiwekea ni wazima kusimamia Sheria ,kanuni na masharti ya ushirika nchini ikiwa ni pamoja na kuwa wanachama hai  aliyelipa nusu ya hisa za uanachama.

Pia alikemea baadhi ya tabia za  wanachama kutumia jazba au ushabiki  katika kuchagua viongozi watakaosimamia ushirika kwani mkifanya hivyo wanamnatinga chama hiki tunachoenda kukizindua leo rasmi kitakufa mikononi mwenu.alisema "Mnatinga inajengwa na nyinyi wanachama wenyewe na mnatatinga itabomolewa na ninyi pia"

Bi Masuba aliwataka wanachama kutumia fursa ya serikali ya awamu ya tano katika kuimarisha ushirika kwani serikali ina nia njema katika kuimarisha ushirika nchini na imeweka mkazo katika usimamizi wa kukuza ushirika wenye nguvu nchini kwa ajili ya maendeleo ya Nchi na kukuza uchumi wa wananchi.

"Kuweni na mipaka katika utendaji kazi wa wanachama na masuala ya kisiasa ili kuepuka migogoro katika chama, vikao vyenu vinawahusu wanachama wenye hisa tuu na sio kila viongozi wa kisiasa, tunapojenga nyumba ni vizuri kuwa na misingi na mipaka"

Akitoa shukrani kwa  wanachama baada ya uchaguzi mwenyekiti wa bodi ya chama cha ushirika cha Mnatinga  Ndg Gerard Ford Richard alisema atatoa ushirikiano kwa bodi iliyokuwepo ili kuendeleza chama, atakua mtii kwa viongozi na wanachama na nitahakikisha hakuna makundi ili kuwaleta wanachama pamoja kama tulivyoanza mwanzo.

Mrajisi Mzaidizi Mkoa wa Ruvuma Bi Bumi Masuba akionesha cheti cha usajili wa chama cha Ushirika cha Mnatinga mbele ya wanachama na wajumbe wa bodi baada ya kufanya uchaguzi wa bodi mpya baada ya bodi ya mpito kumaliza muda wake.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.