• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

SIKU 5 ZA KOMRED ODDO MWISHO WILAYANI TUNDURU.

Imewekwa : July 29th, 2024

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma, Komredi Oddo Mwisho, amefanya ziara ya siku tano mfululizo Wilayani Tunduru kuanzia tarehe 25- 29.07.2024. Ziara hii imekuwa na lengo la kuimarisha uhusiano kati ya viongozi na wananchi, kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, na kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo.

Ujumbe wa ziara hii umekuwa ukiongozwa na Komredi Oddo mwenyewe, akiambatana na viongozi wengine wa ngazi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Kamati ya Siasa Mkoa na Wilaya, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru ambaye amekuwa akiwakilishwa na katibu tawala wa wilaya ya Tunduru ndg. Milongo Sanga, Wabunge wa Majimbo yote ya Tunduru Mhe. Daimu Idd Mpakate na Mhe. Zidadu Kungu,waheshimiwa  Madiwani, Mkurugenzi wa Halmashauri Ndg Chiza Marando na Wataalamu ambao wameshiriki kutoa taarifa za kiufundi na kusimamia utekelezaji wa miradi.

Moja ya shughuli kubwa katika ziara hii imekuwa ni ushiriki katika hafla za mapokezi ya fedha za miradi ya maendeleo katika kata mbalimbali ikiwemo Mtina, Mbati, Ngapa, na Nakapanya. Hafla hizi zimekuwa zikitoa fursa kwa wananchi kuona juhudi za serikali za kuleta maendeleo katika maeneo yao.

Aidha, Katika hotuba zake, Mwenyekiti amekuwa akitumia fursa hii kuzungumza na wananchi katika maeneo mbalimbali kama vile, Mlingoti, Matemanga (ambapo ndipo atamalizia Ziara yake katika Kata hii tarehe 29.07.2024). Katika mikutano hii, amekuwa akisikiliza na kutatua kero za wananchi. Pia, amekuwa akiwataka wananchi kuendelea kushirikiana na serikali katika kuleta maendeleo akiwahimiza kushiriki kikamilifu katika uchaguzi ujao wa serikali za mitaa. Amesema kuwa uchaguzi huu ni fursa kwa wananchi kuchagua viongozi bora ambao wataweza kuwatumikia kwa uaminifu na kuwaletea maendeleo.

Vile vile, mwenyekiti alipata wasaa wa kuzungumza na wakuu wa Idara na vitengo wa Halmashauri, wakuu wa Taasisi mbali mbali katika Wilaya ya Tunduru. Aliwahimiza kujitahidi kutumia ujuzi na utaalamu wao katika kutatua kero za wananchi na kutimiza majukumu yao katika uadilifu ili kuwasaidia wananchi wa Tunduru.

Imetolewa na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru,

Orpa Kijanda,

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.