• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Rais Magufuli Ampa Maagizo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Imewekwa : April 5th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli,

ametoa maagizo kwa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Godfrey Zambi ambaye

pia ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, kuhakikisha ndani ya siku tano soko la

Kata ya Nakapanya wilaya ya Tunduru mkoani humo linafungliwa na kuanza

kutoa huduma kwa  wananchi.


Maagizo hayo aliyatoa jana wakati akizungumza na wakazi wa kata hiyo

muda mfupi baada ya kuwasili mkoani humo kwa ziara  ya kikazi ya siku

tano akitokea mkoa wa Mtwara.


Rais Magufuli alifikia maamuzi hayo baada ya wananchi kutoa kilio chao

cha muda mrefu cha kukosa sehemu ya kufanyia biashara huku wakiwa na

jengo ambalo lilishajengwa kwa kipindi cha miaka saba iliyopita,kwa

madai kuwa jengo hilo lipo karibu na kituo cha Mahakama ya mwanzo.


“Mkuu wa mkoa nataka ndani ya siku tano jengo hili liwe limefanyiwa

uboreshwaji na lianze kutumika ili kuwaondolea adha wananchi waliokuwa

wakiipata kwa muda mrefu sasa”alisema Rais Dkt.John Magufuli.


Aidha katika hatua nyingine Rais Magufuli aliutaka uongozi wa Mahakama

Wilaya ya Tunduru kutafuta eneo lingine la kujenga kituo cha Mahakama

ili kuacha huru eneo hilo kwa shughuli za biashara.


Magufuli ambaye alilazimika kutembelea eneo hilo la soko pamoja na

jengo la kituo cha Mahakama ya mwanzo Nakapanya,ambapo alisema kuna

kila sababu ya kujenga kituo kipya cha Mahakama kutokana na jengo la

awali kuwa na uchakavu.


Hata hivyo akiwa kwenye majengo hayo alitoa shilingi milioni kumi huku

viongozi mbalimbali wakiwemo wabunge walichangia milioni 12 na kufanya

jumla ya shilingi milioni 22 kwa ajili ya ujenzi wa kituo kipya cha

Mahakama.


 Mwisho.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.