• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

NAIBU Waziri wa Maji Afanya Mkutano wa Hadhara na Wananchi.

Imewekwa : November 21st, 2023

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Eng. Maryprisca Mahundi, amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa vijiji vya Mtina,Tinginya, Lipepo, Nalasi na Chilundundu wilaya ya Tunduru.

Mkutano huo ulilenga kusikiliza kero za wananchi kuhusu upatikanaji wa maji. Katika mkutano huo, wananchi walieleza kero mbalimbali wanazokumbana nazo, ikiwemo Ukosefu wa maji ya uhakika, hususani katika maeneo ya vijijini, Maji machafu ambayo hayafai kwa matumizi ya binadamu, na Uharibifu wa vyanzo vya maji.

Mhe. Eng. Mahundi aliahidi kuhakikisha kero zote zinafanyiwa kazi haraka iwezekanavyo. Alisema kuwa Serikali inatekeleza miradi mbalimbali ya maji katika wilaya ya Tunduru, na kwamba miradi hiyo itakapokamilika, itasaidia kutatua changamoto za maji kwa wananchi. Aliahidi kuagiza wataalamu watakaosaidia kuboresha miundombinu ya maji na kuhakikisha kuwa maji yanapatikana kwa uhakika.

"Nimesikia kero mnazokumbana nazo, nami naahidi kuungana na adhima ya serikali ya awamu ya sita chini ya Raisi wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha tunamshusha mama ndoo kichwani inatimia, " alisema Mhe. Eng. Mahundi.”Ninakwenda kuwaagiza wataalamu wangu kuhakikisha kwamba kila kijiji kinafikiwa na maji safi na salama”.

Aidha, Mhe. Eng. Mahundi alikemea wananchi wanaofanya shughuli za kilimo na ufugaji karibu na vyanzo vya maji kuacha mara moja. Alisema kwamba shughuli hizo zinachangia uharibifu wa vyanzo vya maji. Hivyo,alishauri kuwa  wananchi wanapaswa kufanya shughuli hizo kuanzia umbali wa mita 60 kutoka kilipo chanzo cha maji.

Katika mkutano huo Mhe, Eng Mahundi alimpongeza meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Tunduru Eng. Maua Joseph Mgala, kwa kufanikiwa kusambaza maji maeneo ya vijijini kwa asilimia nyingi, vilevile kusimamia vyema na kuhakikisha mradi wa maji vijijini unakamilika kwa viwango na ubora wa juu.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.