• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Naibu waziri OR-TAMISEMI akagua mradi wa upanuzi wa Kituo cha afya Matemanga na Mkasale

Imewekwa : August 15th, 2018

Akiwa katika ziara ya ukaguzi mwenendo wa ujenzi wa majengo katika vituo vya afya Matemanga na Mkasale Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Naibu waziri ofisi ya rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mh.Josephat Kandege alisema serikali imetoa milioni 500 katika kituo cha Afya matemanga na 400 katika kituo cha afya Mkasale ili kuhakikisha kwa huduma za afya zinaboreshwa.

Hayo yamesemwa na Naibu waziri ofisi ya rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mh.Josephat Kandege katika ziara ya ukaguzi wa ukarabati wa miundombinu ya majengo katika kituo cha afya Matemanga mapema wiki.

Akizungumza na viongozi wa mkoa,wilaya pamoja na wananchi wanaozunguka kituo cha afya Matemanga alisema eneo la kituo cha afya Matemanga ni dogo na majengo yake yanakaribiana na makazi ya wananchi hivyo ni vyema serikali kuchukua hatua za makusudi za kulipa fidia stahiki kwa wananchi ili kupisha eneo hilo.

Naibu waziri Kandege amesema majengo ya kituo cha afya kukaribiana sana na wananchi makazi ya wananchi ni hatari wakati wa magonjwa ya mlipuko na hata mionzi inayotoka katika chumba cha mionzi ni hatari kwa afya za wananchi.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya wilaya ya Tunduru Ndg Chiza MArando akisalimiana na Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI  Josephat Kandege akiwa katika ziara ya ukaguzi mwenendo wa ujenzi wa upanuzi wa majengo ya Kituo cha afya  Matemanga.

Akielezea kuhusu eneo la kituo cha Afya Mh. Kandege alisema kuwa eneo la kituo cha afya linatakiwa kuwa na ukubwa wa ekari  nane na kuendelea hivyo ni jukumu la mkoa kushirikiana na halmashauri ya Tunduru kuhakikisha kuwa wanatwaa maeneo kuzunguka kituo hicho.

“viongozi wa mkoa simamieni upatikanaji wa ekari nne zaidi ili kuwe na eneo la ekari nane kulingana na mahitaji ya eneo la ujenzi wa vituo vya afya, wananchi nawaomba kuachia maeneo na serikali ya  kijiji fanyeni mpango wa kuwapatia maeneo mengine”

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Josephat Kandege (wa pili kutoka kushoto) akikagua mtambo wa uliotumiwa na halmashauri katika kufyatua tofali za ujenzi wa majengo katika vituo vya afya Matemanga na Mkasale akiwa katika ziara 

Hata hivyo aliwasisitiza wananchi wa Tunduru kujitokeza kwa wingi kujiunga na mfuko wa bima ya afya jamii iliyoboreshwa (ICHF)  ili kuweza kupata matibabu yenye uhakika kwa kaya watu sita kwa kipindi cha mwaka mzima kwa shilingi elfu 30 tuu. “bima ya afya ya jamii iliyoboreshwa inakuwezesha kupata matibabu katika hospitali ya wilaya, kituo cha afya na hospitali ya mkoa kwa elfu 30 tuu.”

Naibu waziri kandege amehitimisha ziara mkoani Ruvuma katika wilaya ya Tunduru ya kufanya ukaguzi wa ukarabati wa vituo vya afya na kutoa maagizo ya ujenzi wa majengo kulingana na maelekezo yanayotolewa, pia kuhakikisha kuwa kila kituo cha afya kinajenga jengo la mionzi (Ultrasound)  ili kurahisisha upatikanaji wa huduma ya mama wajawazito.

 

Imetolewa na 

Theresia Mallya

Afisa Habari Halmashauri Tunduru

Simu 0764287387

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.