• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MWALIMU NYERERE: MAONO YAKE YANAENDELEA KUIPA MWELEKEO TANZANIA YA SASA

Imewekwa : October 14th, 2025

Imefika miaka 26 tangu Muasisi wa Taifa la Tanzania, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aage dunia, lakini bado misingi, falsafa na dira aliyoiacha inaendelea kuwa mwanga unaoiongoza nchi kuelekea maendeleo endelevu.


Tangu enzi za kupatikana kwa Uhuru, Mwalimu Nyerere alihimiza Watanzania kudumisha umoja, amani na kujitegemea, akiamini kuwa maendeleo ya kweli yanapatikana pale wananchi wanaposhiriki moja kwa moja kuyajenga kwa kutumia rasilimali walizonazo.


Katika moja ya hotuba zake, Mwalimu Nyerere alisisitiza kuwa:


> “Maendeleo lazima yawaguse watu, yawasaidie kuinua maisha yao katika hali ya Uhuru, siyo ya utegemezi.”



Aliwahimiza Watanzania kutumia mali asili, ardhi, madini, gesi, misitu na utaalamu wa ndani kabla ya kutegemea wataalam kutoka nje, akiamini kuwa njia hiyo ndiyo itakayowezesha Taifa kusonga mbele kwa uhuru wa kweli.


Falsafa zake ziliweka msingi wa maendeleo tunayoona leo. Ndoto yake ya kuifanya Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi sasa imetimia; Serikali inatekeleza majukumu yake yote kutoka mjini humo kama alivyotamani. Vilevile, maono yake kuhusu kilimo na viwanda yanaendelea kutekelezwa kupitia sera na mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongoza mapinduzi katika sekta hizo kwa lengo la kuinua uchumi wa wananchi.


Hayati Nyerere aliamini kuwa maendeleo hayana maana kama hayaleti mabadiliko katika maisha ya watu, jambo ambalo linaendelea kuzingatiwa hadi leo kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi.


Serikali imeendelea kutekeleza miradi mikubwa kama vile Reli ya Kisasa (SGR), Mradi wa Umeme wa Mto Rufiji, Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), pamoja na ujenzi wa shule, hospitali, barabara, bandari, viwanja vya ndege na meli mpya — yote ikiwa ni uthibitisho wa kuenzi fikra za Baba wa Taifa kwa vitendo.


Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (2020–2025) pia imeendeleza falsafa hizo kwa kusisitiza kujenga uchumi wa kitaifa unaowanufaisha Watanzania na kuhakikisha rasilimali za nchi zinawanufaisha wananchi wote, si wachache.

Leo hii, tunapomkumbuka Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, tunatambua kuwa mchango wake haukuwa wa maneno pekee, bali ulikuwa wa vitendo vilivyojenga misingi imara ya Taifa.

Mwalimu, tutakukumbuka daima – kwa hekima zako, kwa maono yako, na kwa moyo wako wa kuwatumikia watu.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.