• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

“MSIKATE tamaa, Elimu Haina mwisho”, DSAEO Tunduru.

Imewekwa : December 5th, 2023

Afisa Elimu, Elimu ya watu wazima (DSAEO) wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru, Bi. Mariamu Magulima, amefanya kikao maalumu cha kuwapongeza na kuwatia moyo wanafunzi waliohitimu na wanaoendelea na masomo yao tarehe Decemba 05 katika kituo cha Mlingoti TRC wilayani humo.

Akizungumza katika kikao hicho Bi.Magulima,alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwakumbuka watoto wa kike waliokatisha masomo yao kwa sababu mbalimbali, kuamua kuwarejesha shule ili kupata haki yao ya msingi ya Elimu, na pia aliwasisitiza wanafunzi hao kutokukata tamaa, aliwaomba kuwa mabarozi wazuri kwa wenzao ambao bado hawajajiunga na elimu hiyo,na kwamba bado wanayo nafasi ya kutimiza ndoto zao kupitia Elimu.

“Ninyi ni darasa ambalo lipo mikononi mwa serikali, kufanya mtihani wa kufuzu (Qualifying Test-QT) ni hatua kubwa sana katika kuelekea kutimiza na kuziishi ndoto zenu katika kupata elimu bora” alisema Bi.Magulima “kupitia ninyi tunataka kuona idadi ya wanafunzi wanaojiunga inaongezeka Zaidi,hata pale mnapokuwa mmehitimu elimu yenu msisite kufika katika ofisi zetu ili tuwapatie ushauri zaidi wa jinsi ya kujiunga na masomo ya elimu ya juu Zaidi”

Katika halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, mradi huu ulianza rasmi mwaka 2022 mwezi Januari, ambapo kituo cha Mlingoti TRC kilifanikiwa kusajili wanafunzi 19 na wote walifanya mtihani wa kufuzu (Qualifying Test-QT), wanafunzi wawili tu ndio walifanya vizuri na kufanikiwa kuingia hatua ya pili, yaani kidato cha III na IV, ambao mwaka huu (2023) wamefanya mtihani wao wa utimilifu wa kidato cha nne.

Aidha, mpaka sasa kituo cha Mlingoti TRC kimefanikiwa kusajili wanafunzi 15 wa hatua ya kwanza na wote wamekwisha fanya mtihani wa kufuzu (Qualifying Test-QT), wanafunzi hawa wataaanza masomo yao mwaka wa masomo utakaoanza Januari, 2024.

SEQUIP (Secondary education Quality Improvement Project), ni Miradi maalumu ya kitaaluma inayosimamiwa na OR-TAMISEMI chini ya Taasisi ya Elimu ya watu wazima, yenye lengo la kuwaendeleza wanafunzi wa kike waliokatisha masomo yao ya sekondari katika mfumo rasmi, kwasababu mbalimbali zikiwemo ujauzito, hali ngumu ya maisha, maradhi ya kudumu na nyinginezo. Aidha, Serikali inagharamia masomo ya wanafunzi hawa kwa asilimia zote.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.