• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MRADI wa Kijana Jiongeze kuinua michezo Tunduru.

Imewekwa : October 18th, 2023

Asasi ya kiraia COUNSENUTH ambao ni wasimamizi wa utekelezaji wa mradi wa Kijana Jiongeze kwa kushirikiana na Halmashauri kupitia ufadhili wa MasterCard Foundation imekabidhi vifaa vya michezo kwa shule 23 za Sekondari zilizopo Wilayani Tunduru.

Akikabidhi vifaa hivyo katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Bi. Edina Obed Mgunda, ambaye ni Mratibu wa Mradi wa Kijana Jiongeze awamu ya pili, amesema vifaa hivyo vya michezo ni kwa ajili ya utekelezaji  wa shughuli za mradi huo katika kuchangia jitihada za shule za Serikali ili kuboresha michezo mashuleni, na hivyo, kuboresha hali ya mahudhurio na utayari wa kusoma na kupenda shule.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru (Kulia) Ndg. Chiza Marando akikabidhiwa Vifaa vya Michezo na Mratibu wa Mradi wa Kijana Jiongeze Bi. Edina Mgunda

“Mradi umepanga kufanya mashindano ya michezo na taaluma katika shule za Sekondari 23 ambazo mradi huu unatelekezwa”. Alisema “Vifaa hivi vya Michezo vitaongeza chachu ya wanafunzi kupenda shule, lakini pia kupenda Elimu, sisi kama wadau wa Elimu tunaamini kuwa michezo inaweza kuongeza kujifunza na kumvutia mwanafunzi kubaki shuleni” Alisema.

Vifaa vya michezo vilivyokabidhiwa ni Seti 14 za Jezi na mipira 46, ambapo, Seti saba za jezi ni kwa ajili ya timu saba za mpira wa miguu na saba kwa mpira wa pete, mipira 23 ni kwa ajili ya mpira wa miguu na 23 mpira wa pete.

(kushoto) Afisa Elimu Sekondari Mwal. Patrick Haule akipokea Vifaa vya Michezo

COUNSENUTH kwa kushirikiana na Idara ya Elimu Sekondari ya Wilaya ya Tunduru inatekeleza mradi wa KIJANA JIONGEZE wenye lengo kuu la kukabiliana na changamoto za ufaulu wa na kuhusisha njia za kuwawezesha wasichana kuwa na stadi za maisha zitakazowasaidia kutambua uwezo wazo, kujiamini na kuwaandaa kwa ajili ya ajira na kujiajiri. Mradi huu unatekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, kwa ufadhili wa MasterCard Foundation.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.