• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Mnada

Imewekwa : November 2nd, 2017


Msimu wa Korosho waanza kwa kishindo Wilayani Tunduru.

Msimu wa ununuzi wa zao korosho wilayani Tunduru kwa mwaka 2017/2018 umeanza kwa kasi nzuri ya mnada wa kwanza kufunguliwa  mapema leo katika Kijiji cha Namakambale tarafa ya Nakapanya mkoa wa Ruvuma na mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh. Juma Zuberi Homera.

 Ununuzi  na uuzaji wa zao la  korosho  umeanza kwa kasi nzuri  ukilinganisha na miaka mingine kwa  bei ya juu kwa kilo tsh 3,950 kwa mnada wa leo wa tarehe 02/11/2017, ikiwa ni bei kubwa kwa msimu huu toka uanza.

Jumla  ya wafanyabiashara waliowasilisha  zabuni (tender)  ni 17 lakini walishiriki katika mnada  ni 14 za wanunuzi kutoka ndani na nje ya nchi na  kampuni ya Korosho Africa Ltd ndio iliyoshinda tenda leo kwa kununua kilo 544,000 kwa Ths 3,950 sawa na Tan 544 za korosho ghafi  zilizokuwa ghalani ni  kilo 544,144.

Akifungua mnada wa leo mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika wilayani Tunduru TAMCU ltd Ndg Hashim Twalib Mbalabala alisema zoezi hili linafanyika kwa uwazi ili kuondoa migogoro miongoni mwa wakulima, serikali na vyama vya msingi.

Aidha akisoma taarifa kabla ya mnada afisa ushirika wilaya Ndg Peter Malekela alisema makato ya kisheria yatakatwa ikiwa ni ushuru wa Amcos sh 90, Mfuko wa wakfu -CDTIF sh 10, ushuru wa Halmashauri 43.5, mchango wa Elimu sh 50 na gharama za usafiri sh 50.


Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh.Juma Zuberi Homera akiongea na wananchi wa wilaya ya Tunduru katika ufunguzi wa mnada wa kwanza wa korosho uliofanyika katika kijiji cha Namakambale wilaya ya Tunduru mkoa wa Ruvuma

Mkuu wa wilaya ya Tunduru ambaye alikuwa mgeni wa heshima katika ufunguzi wa mnada wa kwanza alisema bei ni kubwa toka msimu umeanza na korosho leo imeuzwa kwa bei ya shilingi 3950 ikiwa ni ongezeko la shilingi 200 ya bei ya msimu ulipita ambapo mnada wa kwanza ulinzakwa shilingi 3750.

Aidha Mh. Homera alimshukuru rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli kwa kuwezesha na kuramisha mfumo wa stakabadhi ghalani na kutoa kipaumbele kwa zao la korosho kuwa la biashara.

“Naishukuru serikali kutoa wigo mpana kwa zao la korosho na kuwa la kipaumbele na pia kuruhusu wanunuzi kutoka nje ya nchi kuja kununua korosho yetu”

Na kwa upande wa wananchi wa Kijiji cha Namakambale wameomba kuongezwa kwa magari ya kusafirisha korosho kutoka katika vyama vya msingi na kupeleka na ghala kuu la Tamcu lililopo Tunduru mjini.

Afisa Ushirika Wilaya Ndugu Peter Malekela wakisoma Tenda za wanunuzi wa Korosho mara baada ya kufunguliwa kwa sanduku la Tenda leo katika mnada wa kwanza uliofanyika katika kijiji cha Namakambale wilayani Tunduru

Hata mnada huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa wilaya ya Tunduru wakiongozwa na mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh. Juma Zuberi Homera , kaimu Mkurugenzi Mtendaji (W) Ndg Chiza Marando ambaye ni Afisa Kilimo Wilaya, Mwenyekiti wa chama Kikuu cha Ushirika Tunduru (TAMCU) Bw Hashim Twalib Mbalabala na wananchi. 

  

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.