• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC Mtatiro afanya ziara siku 3 kufuatilia udahili kidato cha kwanza

Imewekwa : January 27th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Wakili Julius S. Mtatiro amefanya ziara ya siku tatu ya kikao kazi kuanzia tarehe 25-27 mwezi Januari 2024 kufuatilia hali ya udahili wa watoto shule za sekondari zilizopo wilayani Tunduru. Ziara hiyo ilihusisha Afisa Tarafa wote, watendaji kata, Afisa Elimu kata wote, na wakuu wa shule za Sekondari katika wilaya nzima.

Mhe. Wakili Mtatiro alieleza kuwa anasikitika kuona kuwa bado kuna idadi kubwa ya wanafunzi ambao bado hawajaandikishwa shule za sekondari. Aliwataka watendaji kata na Afisa Elimu kata  wote kusimamia kikamilifu udahili wa wanafunzi katika kata zao.

Aliwataka watendaji kata kutengeneza utaratibu maalumu wa kuzifikia familia na wazazi au walezi wote ambao bado hawajapeleka watoto shule na kuhakikisha watoto wote ambao hawajaandikishwa wanaanza masomo mara moja. Wakifanya kazi kwa kushirikiana wataweza kuboresha hali ya udahili wa watoto shule za sekondari katika wilaya ya Tunduru.

Pichani:Baadhi ya Wakuu wa Shule, Afisa Elimu kata na Watendaji wa Kijiji wa Wilaya ya Tunduru.

“Ninashangazwa na kusikitishwa na idadi ndogo ya wanafunzi ambao wameandikishwa shuleni mpaka sasa, Watendaji kata na Afisa Elimu kata Shirikianeni na polisi kata ili kuhakikisha watoto wote ambao hawajaandikishwa shule mpaka sasa wanapelekwa shule” Alisema “Msipochukua hatua za haraka kuhakikisha watoto hawa wanapelekwa shule, mimi nitawachukulia hatua za kisheria ninyi”.

Mhe. Wakili Mtatiro alitoa agizo kuwa watoto wote ambao hawajaandikishwa watafutwe na waandikishwe shuleni, kwani elimu ni haki yao ya msingi. Alisisitiza kuwa mzazi yoyote ataye kiuka agizo lake achukuliwe hatua mara moja.

Aidha, aliwataka Wakuu wa Shule kuandaa utaratibu mzurii wa kuwapokea wanafunzi ambao utawasaidia kuwafuatilia kwa ukaribu kulingana na taarifa zao, aliongezea kuwa wanapaswa kushirikiana na serikali ya kijiji katika zoezi la kuwapokea wanafunzi hao ili kusiwepo na changamoto yoyote.

Ziara ya Mhe. Mkuu wa Wilaya inaonyesha kuwa serikali inatambua umuhimu wa elimu ya sekondari, ziara hiyo pia inaonyesha kuwa serikali inachukua hatua za kuboresha upatikanaji wa elimu ya sekondari kwa watoto wote wa Tanzania, kwa kuhakikisha inatengeneza miundombinu bora inayowezesha wanafunzi kupata masomo yao katika mazingira bora.  

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.