• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MKURUGENZI MARANDO AAGIZA MIRADI YOTE IKABIDHIWE IFIKAPO TAREHE 01 MACHI, KAZI IFANYIKE USIKU NA MCHANA.

Imewekwa : February 3rd, 2026

MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, Ndugu Chiza Marando, amefanya ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo tofauti ya wilaya ya Tunduru, kwa lengo la kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Katika ziara hiyo, Mkurugenzi Marando aliwataka mafundi, Mafundi Ujenzi na wasimamizi wote wa miradi kuhakikisha wanaharakisha utekelezaji wa kazi kwa kuzingatia viwango vilivyokubaliwa, huku akisisitiza kuwa miradi yote inapaswa kukamilika na kukabidhiwa rasmi ifikapo tarehe 01 Machi. Alitoa maelekezo kuwa kazi ifanyike usiku na mchana ili kufikia muda uliopangwa.

Aidha, alitoa onyo kali kuwa hatovumilia uzembe wa mtaalamu au fundi yeyote atakayesababisha ucheleweshaji wa kukamilika kwa miradi hiyo, na kusisitiza kuwa hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya wote watakaokiuka maagizo hayo, ili kulinda thamani ya fedha za umma na maslahi ya wananchi.


Miradi iliyotembelewa na kukaguliwa katika ziara hiyo ni pamoja na ujenzi wa shule ya awali na shule ya msingi katika Kijiji cha Majimaji, ujenzi wa vyumba vya madarasa pamoja na matundu ya vyoo katika Shule ya Msingi Ruanda, ukamilishaji wa zahanati zilizopo katika vijiji vya Sauti Moja na Songambele, pamoja na mabweni yaliyopo katika Shule ya Sekondari Nakapanya ambayo kwa sasa tayari yanatumika.


Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru katika kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuhakikisha inakamilika kwa wakati, kwa ubora unaotakiwa na kwa manufaa ya wananchi wa Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MARANDO AAGIZA MIRADI YOTE IKABIDHIWE IFIKAPO TAREHE 01 MACHI, KAZI IFANYIKE USIKU NA MCHANA.

    February 03, 2026
  • HATUA MADHUBUTI TUNDURU: MKURUGENZI MTENDAJI AWEKA MIKATABA KWA WASIMAMIZI WA MIRADI

    February 02, 2026
  • MKUTANO WA KAWAIDA BARAZA LA MADIWANI WA PITIA TAARIFA ZA KATA WAENDELEA TUNDURU

    January 29, 2026
  • NUKUU YA LEO

    January 26, 2026
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.