• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Maafisa Mawasiliano Serikalini Wapewe Nafasi

Imewekwa : July 25th, 2018

Hayo yamesemwa na kamati  ya ufuatiliaji inayofanya ukaguzi wa utendaji kazi wa maafisa habari/ Mawasiliano katika taasisi mbalimbali za serikali, kufuatia maagizo yaliyotolewa katika mkutano wa 14 wa maafisa habari na mawasiliano serikalini ulifanyika jijini Arusha mwezi machi 2018 ya kuwataka chama cha Maafisa Mawasiliano Serikali (TAGCO) kushirikiana na Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali kufanya ziara ya katika ofisi za maafisa mawasiliano ili kuchochea utendaji kazi wao.

Akiwasilisha ujumbe huo katika ofisi ya Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Tunduru kiongozi wa msafara kutoka Ofisi ya Msemaji mkuu wa serikali Ndg Casmiri Ndambalilo alisema kazi kubwa ya maafisa mawasiliano ni kuisemea serikali  inavyotekeleza majukumu na kuleta uwazi kwa wananchi inayowahudumia.

Aidha alisema ili waweze kutekeleza majukumu ya mawasiliano ya  kimkakati  kuisemea serikali ipasavyo, halmashauri inatakiwa kuwawezesha vitendea kazi, kuwashirikisha katika vikao vya maamuzi na kupewa rasimali za kuitembelea  miradi inayotekelezwa ndani ya taasisi zao.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Tunduru Ndg Chiza Cyprian Marando aliwapongeza kufika kufanya ufuatiliaji kwani serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mh.John Pombe Magufuli inahitaji ukweli na uwazi   na ili wananchi waweze kujua serikali yao inafanya nini ni lazima kutoa taarifa za mara kwa mara kwa wananchi kupitia vyombo vya Habari.

Ndg Chiza Marando alisema “ halmashauri ya Tunduru haikuwa na Afisa Habari kwa kipindi kirefu sana, na mtu muhimu sana ambaye tulitamani kuwa naye na toka alipofika tumejitahidi kupamtia vitendea kazi, na kumshirikisha vikao vyote vya maamuzi, na hata kwenye ukaguzi wa miradi anashirikishwa vizuri , hivyo anaifahamu halmashauri vizuri.”

Hata hivyo walimpongeza Kaimu  Mkurugenzi halmashauri ya Tunduru kwa kutambua umuhimu wa Afisa Mawasilaino katika taasisi yake na kutekeleza kwa wakati maagizo yaliyotolewa na viongozi ikiwa ni pamoja na kununua  vitendea kazi kwa ajili ya Ofisi ya Habari, Ushirikishwaji wa Afisa Habari katika vikao vya maamuzi.

pamoja na pongezi hizo Kamati ya Ufuatiliaji kutoka Ofisi ya Msemaji Mkuu wa serikali na Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini walimtaka Afisa Habari kutumia fursa aliyoanayo kutoa taarifa mbalimbali za halmashauri yake kupitia Idara ya Habari maelezo  ajili ya kutangaza katika vyombo vya Habari.

Imtolewa na

Theresia Mallya

Afisa Habari Halmashauri.

25/07/2018

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.