• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Maadili ya Walimu

Imewekwa : November 11th, 2017

   

Tume ya Utumishi wa Walimu Rudisheni Maadili ya Walimu.Dkt Ndumbaro.

Hayo yamesemwa katika kikao cha Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt Laurean Ndambaro akiwa katika ziara ya kuwakumbusha watumshi wa umma muelekeo wa serikali ya awamu ya tano katika kujenga misingi ya utumishi wa umma.

Aidha alisema serikali inatarajia kuwa na watumishi wenye uadilifu uliotukuta katika jamii na utoaji huduma kwa wananchi, watumishi wanaowajibika kwa serikali nawananchi, nidhamu ya kazi  kufanya kazi kwa juhudi na maarifa, ndio dira ya serikali na itasimamia kuona kuwa utekelezaji unafanyika.

Dkt. Ndumbaro alisema kufuatia kuwepo na malalamiko mengi katika ofisi yake anaugiza uongozi wa tume ya kusimamia maadili ya walimu Nchini TSC kuhakikisha kwamba nidhamu ya walimu inarudi na kada hiyo kuheshimika kama ilivyokuwa hapo awali.

Dkt. amesema watumishi wanatakiwa kufuata sheria , kanuni na Taratibu za Umma na kuacha kuiabisha serikali kwa kuchukua mikopo iliyopitiliza kwani serikali imeweka sheria ya mtumishi kukopa isiwe zaidi ya 1/3 ya mshahara wake anaopokea ili aweze kumudu maisha na kuendelea kutekeleza majukumu yake.

 “kumukuwa na tabia ya walimu kukopa kupitiliza hata baada ya serikali kuweka sheria ya kiwango cha kukopa kisizidi 1/3 ya mshahara anaopokea wameamua kuhamia katika makampuni yanayokopesha fedha na kupeleka hadi vitambulisho vya benki na nyaraka nyingine kwa udhamini, hali hii  inadhoofisha uwajibikaji na kuharibu nidhamu ya kazi”

Aidha dkt. Ndumbaro ameigaiza tume ya kushughulikia maadili ya walimu nchini TSC kushghilikia masuala ya walimu kikamilifu na kuacha kuingiza siasa katika kazi na kama mtumishi amefanya kosa basi aadhibiwe kulingana na kosa alilofanya. “niwaombe makatibu wa TSC nchini kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyowekwa na serikali katika kushughulikia kesi za walimu”

Dk Ndumbaro aliendelea kusema kuwa ni jukumu la kila mkuu wa Idara na kitengo kusimamia sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma ili kuweza kuleta maendeleo chanya kwa watu anawasimamia na kuondoa kero na malalamiko yanayojitokeza mara kwa mara kwani kuna matatizo mengine ni madogo ambayo yako ndani ya uwezo wa mkuu wa idara au kitengo kuweza kuyatatua.

Aidha dk Ndumbaro alisema ni vyema Halmashauri kujiwekea utaratibu wa kuwapongeza watumishi wanaotimiza wajibu wao vizuri ili kuongeza morali ya utendaji kazi kwa watumishi na kwa wale wanaokiuka maadili ya utumishi na kuwa wazembe katika kazi kupewa onyo kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa Umma.

Dkt.Ndumbaro alisema suala la uhamisho kwa watumishi kutoka katika kituo kimoja cha kazi kwenda kingine wa lipo ndani ya uwezo wa mkuu wa  taasisi na hakuna sababu yoyote ya msingi ya kuzuia uhamisho huo baada ya mtumishi kukidhi vigezo vyote muhimu na  kama mtumishi huyo yupo mmoja mkuu wa taasisi anatakiwa kutoa maoni ya kupewa mtumishi mwingine na sio kuzuia uhamisho.

“nimekuwa nikipokea malalamiko mengi katika ofisi yangu kuhusu wakuu wa taasisi na wakuu wa idara na vitengo kuwazuia baadhi ya watumishi kuhama kutoka kituo kimoja cha kazi kwenda kingine, hii haki ya mtumishi na ni wajibu wa serikali vilevile kumpelaka mtumishi mwingine kwenda kuziba nafasi iliyoachwa wazi”dkt ndumbaro alisisitiza

Watumishi wa Umma waliopo katika wilaya ya Tunduru wakimsikiliza katibu Mkuu Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma Dkt.Laurean Ndumbaro katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa skyway Tunduru tarehe 10/11/2017.

Dkt. Alisema katika kipindi cha mwezi novemba sekrikali italipa madeni ya mishahara ya watumishi, kupandisha vyeo na madaja na ongezeko la mshahara kwa watumishi wote wa umma waliofikia vigezo kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

Kwa upande wa mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Zuberi Homera alimshukuru katibu mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma kufanya ziara katika wilaya ya Tunduru na kuweza kusikiliza changamoto wanazokumbana nazo watumishi katika kutekeleza majukumu yao ya kila katika maeneo yao ya kazi.

Mkuu wa wilaya Homera alisema kuwa Tunduru ina upungufu mkubwa wa watumishi hasa katika sekta ya Afya ambayo kuna mganga mmoja tuu  huku wakiwa na mahitaji ya waganga 28 ili kuweza kutoa huduma, na kuna baadhi ya zahanati hazina kabisa watumishi na zilifungwa kwa muda kutokana na uhaba wa watumishi katika idara ya afya.

“tunaomba wilaya ya Tunduru iangaliwe kwa jicho la pili katika ikama ya watumishi kwani kuna upungufu mkubwa sana ukilinganisha idadi ya watumishi na ukubwa wa eneo la kiutendaji na huduma zinazohitajika kwa jamii”

Hata hivyo katika shule zetu kuna upungufu mkubwa wa walimu ambapo unakuta kuna baadhi ya kuna walimu wawili hadi watano ndio wanafundisha kuanzia darasa la awali hadi darasa la saba, hali hii inapekelea kiwango cha ufaulu kushuka na mwalimu kuwa mzigo mzito sana alisema Mkuu wa wilaya.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Zuberi Homera akifungua kikao na kumkaribisha katimu mkuu ofisi ya Rais Utumish wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro kuongea na watumishi wa wanahudumu katika wilaya hiyo

Alimalizia kwa kuwapongeza watumishi wa Halmashauri ya Tunduru kwa uwajibakaji na utendaji wao kazi uliotukuka na kuwataka kuendelea na moyo huo huo wa kuwatumikia wananchi wa Tunduru ili kuweza kuleta maendeleo kwa wananchi kuloingana na sekta zao.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.