• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Kituo cha afya Nakayaya

Imewekwa : November 27th, 2017


Jumla ya shilingi milioni 11 zimetolewa na kiwanda cha kubangua korosho cha Korosho afrika  kilichopo katika wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma kuchangia ujenzi wa kituo cha afya katika kijiji cha Nakakaya, kituo hiki cha afya kinajengwa kwa mchango wa serikali na mchango wa wafanyabisha wa wilayani Tunduru.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa kituo cha afya Nakayaya kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Kassimu Majaliwa Mb, alipotembelea kukagua ujenzi wa kituo hicho , Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wilaya Ndg Chiza C Marando alisema kuwa mradi huu umeibuliwa na mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera mwaka jana na utatarajiwa kugharimu jumla ya shilingi bilioni 1.6 hadi kukamilika.

Na mpaka hapa kilipofikia ni mchango kutokana na wafanyabiasha waliopo katika wilaya ya Tunduru na wadau wengine wa maendeleo ndio waliotoa michango yao ya mchanga, vifaa vya kiwandani na fedha taslimu baada ya mkuu wa wilaya kuwashikisha wameonesha muamko wa uchangiaji.

Waziri Mkuu afanya ukaguzi wa kituo cha Afya Nakayaya

Akiongea na watumishi, viongozi na wananchi wa kata ya Nakayaya baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Kaasimu Majaliwa amesema kutokana na ongezeko la watu katika wilaya ya Tunduru huduma za afya zinatakiwa kupanuliwa, hivyo nawapongeza viongozi wa wilaya kwa kuanza kutekeleza miradi yenye tija kwa wananchi.

Waziri mkuu amesema nimesikia katika taarifa ya wilaya kuwa hospitali ya wilaya imelemewa na wagonjwa  kutokana onegezeko la watu, pia kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa barabara katika kiwango cha lami kumesababisha kuwa na ongezeko kubwa la magari hivyo ni vyema kupanua huduma za afya pia.

Waziri mkuu Kassimu Majaliwa alisema viongozi wa wilaya waendelee kuwashikirisha wananchi hata wa kawaida kuchangia ujenzi wa kituo hicho ili kiweze kukamilika kwa wakati na serikali kupitia wizara ya afya italeta wataalam wa kutoa huduma katika kituo hicho mara kitakapokamilika.

“Serikali imeweka kipaumbele katika kuwahudumia wananchi na katika ilani ya chama cha mapinduzi imepanga kila kata kuwa na kituo cha afya lakini pia kila kijiji kujenga zahanati katika kuboresha huduma za afya kwa wananchi”alisema waziri mkuu.

kaimu Mkurugenzi chiza Marando Akitoa taarifa ya ujenzi wa kituo cha afya Nakayaya kwa waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Kassimu Majaliwa wakati akiwa ziarani wilayani Tunduru

Akipokea hundi yenye thamani ya shilingi milioni 11 iliyotolewa na kiwanda cha kubangua korosho Tunduru cha  Korosho Afrika kwa ajili ya kuchangia uendelezaji wa ujenzi waziri mkuu  Kassimu Majaliwa aliushukuru uongozi wa kiwanda hicho kwa kuchangia huduma za jamii katika wilaya ya Tunduru.

pia aliwashurukuru wabunge wa wilaya ya Tunduru kwa kumuunga mkono katika kuchangia ujenzi wa kituo hicho ambapo jumla ya shiling milioni 32, bati 50 na mifuko ya saruji 150 viliadiwa na wabunge wa Tunduru Kaskazini Eng Ramo Makani, Tunduru Kusini Mh Daimu Mpakate na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Ruvuma Mh Sikudhani Chikambo pamoja na mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bi.Christina Mndeme.

Waziri mkuu Kassimu Majaliwa alisema serikali inaendelea kuimarisha huduma za afya na wilaya ya Tunduru ipo katika mpango wa uboreshaji wa vituo vya afya vya Mkasale na Matemanga ambavyo vimetengewa bilioni moja, yaani milioni 500 kwa kila kituo cha afya za kuboresha majengo ya kutolea huduma.

waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akionesha hundi ya m

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.