• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KILELE cha maadhimisho Siku ya UKIMWI Mkoa wa Ruvuma

Imewekwa : December 1st, 2023

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yamefanyika leo Desemba mosi, ambapo maadhimisho hayo kwa Mkoa wa Ruvuma yameadhimishwa Wilayani Tunduru.

Maadhimisho hayo yaliambatana na shughuli mbalimbali ikiwemo upimaji wa VVU na kifua kikuu, utoaji wa elimu ya afya ya uzazi na Lishe, na utoaji wa huduma za ushauri nasaha na kupima pamoja na Michezo mbalimbali ikiwemo Mpira wa Miguu.

Akizungumza mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani , Mhe.Wakili, Julius S. Mtatiro , ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, aliwataka wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kuendelea kujikinga na maambukizi ya VVU kwa kutumia njia salama za kujikinga zinazoshauriwa na wataalamu wa Afya.

“Maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi bado ni tatizo kubwa katika Mkoa wetu huu wa Ruvuma,” alisema “Wanaume tunapaswa kuhudhuria vituo vya afya ili kuweza kutambua afya zetu, Ni wajibu wa kila mwananchi kutambua afya yake ili aweze kujikinga na maambukizi na vile vile kuwalinda wengine”.

Aidha, akisoma taarifa ya mganga mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Daktari, Louis chomboko  ya ugonjwa wa UKIMWI mkoani humo, Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa Bi. Mariamu Juma, alisema kuwa, asasi za kiraia zuchukue fursa ya kuelimisha na kuhamasisha watu kupitia huduma za afya kufanya ubunifu, kujenga uaminifu, kufanya ufuatiliaji na utekelezaji wa sera na afua za huduma mbalimbali na kusimamia uwajibikaji wa kila mmoja wetu.

Pichani: Ni Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa, Bi. Mariamu Juma, akisoma taarifa ya mganga mkuu ya ugonjwa wa UKIMWI mkoa wa Ruvuma.

Takwimu zilizosomwa katika taarifa ya mganga mkuu wa mkoa wa Ruvuma zinaonyesha kuwa, Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa 14 yenye asilimia kubwa ya maambukizi ya VVU kitaifa ukiwa na una asilimia 5.6, ambapo kiwango cha maambukizi kitaifa ni 4.7 kwa matokeo ya viashiria vya UKIMWI Tanzania yam waka 2016/2017. Aidha, kiwango hiki cha maambukizi kimepungua kutoka asilimia 7 mwaka 2011.

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ikiwa ni “Jamii iongoze kutokomeza UKIMWI”, kauli mbiu hii  inaangazia umuhimu wa kutoa  nafasi kwa jamii kushika hatamu katika kutokomeza UKIMWI.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.