• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KAMPENI ya utunzaji Mazingira Yapata kasi Wilayani Tunduru

Imewekwa : March 23rd, 2024

KAMPENI ya Utunzaji Mazingira Yapata Kasi Wilayani Tunduru.

Shirika la Uhifadhi wa Mazingira na Maliasili Duniani (WWF),limeendesha kampeni ya saa moja la utunzaji wa mazingira (60 Earth Hour) katika, Kata ya Sisi kwa Sisi, Kijiji cha Sisi kwa Sisi Katika Shule ya Msingi Mahauhau  Wilayani Tunduru.

Kupitia kampeni hii ya  saa moja iliyotolewa kwa upandaji wa miti imekuwa ishara na azma ya kuendeleza jitihada za kutunza mazingira, ambayo ni sehemu ya kampeni ya Utunzaji Mazingira Duniani inayofanyika kila mwaka ifikapo Machi 23.

Akizungumza baada ya zoezi la upandaji miti, Ndg. Deogratius Kilasara, Afisa Uhifadhi kutoka WWF, ameeleza kuwa lengo kuu la zoezi hili ni kuhamasisha utunzaji wa mazingira. Amesisisitiza kuwa jitihada za kutunza mazingira zinapaswa kuwa endelevu na ni jukumu la kila mmoja katika jamii.

“Tuondokane na zana ya kuwa, utunzaji wa Mazingira ni wa kundi Fulani pekee, bali tujjue kuwa kutunza mazingira ni jukumu la kila mmoja katika Jamii”. Alisema Kilasara.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mahauhau, Bi. Rozina Ngonyani, ameeleza mikakati yao ya kuhakikisha wanatunza mazingira kwa uangalifu, ikiwa ni pamoja na kuendelea kufuatilia ukuaji wa miti ili kuhakikisha manufaa yake yanadumu.

Kwa upande wake, Faraja Mussa, mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mahauhau, ameishukuru WWF kwa kuwawezesha kushiriki katika jitihada za utunzaji wa mazingira na ameahidi kuchukua jukumu hilo kwa uzito, akiahidi kuwa mstari wa mbele katika kuelimisha na kusaidia jamii katika utunzaji wa mazingira.

Kaimu Afisa Maliasili na Hifadhi za Mazingira, Ndg. Dunia Almasi, ameishukuru WWF kwa ushirikiano wao katika jitihada za kutunza mazingira. Amesema mazingira ni nyenzo muhimu katika uhai wa binadamu na ametoa wito kwa jamii kushirikiana katika kuhifadhi mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Kampeni hii imeleta matumaini mapya kwa jamii ya Sisi kwa Sisi na imeonyesha umuhimu wa ushirikiano katika kudumisha mazingira safi na endelevu.

Kampeni Hiyo imeenda sambamba na Kauli mbiu isemayo #Earth hour BiggestHourForEarth

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.