• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

JUKWAA la Wanawake lazinduliwa Tunduru.

Imewekwa : September 21st, 2023

Jukwaa la Wanawake  Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma limezinduliwa  tarehe 21 September 2023 likiwa na lengo la kuwapa fursa na kuwapambania wanawake waweze kujiimarisha kiuchumi na kujikwamua na kipato duni.

Akihutubia Jukwaa hilo Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mheshimiwa Julius Mtatiro, alisema Jukwaa hili likiwezeshwa kikamilifu litakua msingi wa kutatua changamoto mbalimbali, kwasababu katika falsafa ya uchumi mwanamke ana uwezo mkubwa wa kutunza Fedha, ni vyema kuwepo na uchumi shirikishi ndani ya familia.

“Jukwaa hili halijazinduliwa kwa maamuzi ya mtu mmoja, uundwaji wake ni maagizo ya mikataba mbalimbali pamoja na sheria ambazo zinalinda maslahi ya mwanamke wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali inapinga vikali ndoa za utotoni, Binti aachwe asome”. Alisema.

Pichani (Aliyesimama): Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mh. Julius Mtatiro.

Kwa upande wake Katibu wa jukwaa la wanawake Mkoani Ruvuma Mwl. Neema Kajange alisema, Mama ni mlinzi mkubwa wa familia na ili kumfikia mwanamke wa chini kabisa Halmashauri zitenge kifungu kitakachosaidia kuwaunganisha na kushiriki katika majukwaa yanayohamasisha shughuli za uchumi na uzalishaji mali.

Pichani: Katibu wa Jukwaa la Wanawake Mkoani Ruvuma Mwl. Neema Kajange.

Aidha, Mwenyekiti wa Jukwaa la wanawake Wilayani Tunduru Bi. Somoe Singizi amewasisitiza wanawake Wilayani humo kushirikiana katika kutokomeza mfumo dume katika familia, aliongezea kusema, Wanawake ni jeshi kubwa hivyo ni jukumu la kila mmoja wao kujituma na kufanya kazi kwa bidii.

Pichani: Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Wilayani Tunduru Bi. Somoe Singizi.

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum linasimamia, kutoa miongozo ya uanzishaji na uendeshaji wa Jukwaa la uwezeshaji wa wanawake kiuchumi ikiwa ni jitihada  za kuhakikisha  kuwa mipango  ya Serikali  inalenga katika kumwezesha mwanamke kiuchumi ili kukuza uchumi na kuleta maendeleo stahimilivu kwa wanawake wa Taifa kwa ujumla.

Pichani (kuli): Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mhe. Mtatiro akikagua bidhaa za maonesho.

Kauli mbiu ya Jukwaa la Wanawake Mwaka 2023 ni “Mfumo Dume katika familia ni hatari kwa uchumi wa Mwanamke”.


Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.

 

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.