• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Bazara la Madiwani Tunduru lapitisha bajeti ya Bilioni 36.8

Imewekwa : February 14th, 2019

Halmashauri ya Wilaya Tunduru inatarajia kutumia bilioni 36,899,337,707.08 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020, kati ya fedha hizo bilioni 2,641,184,396.00 mapato ya ndani, ikiwa mapato halisi Tsh 2,033,064,396.00 na mapato ya ndani mengineyo ni Tsh 608,120,000.00, pamoja na hayo ruzuku ya mapato mengineyo na mishahara imepanga kutumia Tsh 29,910,702,566 na Tsh 4,147,450,745.08 zitatumika katika miradi ya maendeleo kutoka serikali kuu.

Akiwasilisha rasimu ya bajeti ya mwaka 2019/2020 mbele ya baraza la madiwani kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji  Afisa Mipango halmashauri ya Tunduru Ndg Jumanne Mwankhoo alisema  maandalizi yamezingatia vipaumbele vilivyotajwa katika mwongozo wa bajeti ya serikali za mitaa kwa mwaka 2019/2020.

Vipaumbele vya bajeti ni kukamilisha miradi viporo ili kuongeza upatikanaji wa huduma hususani katika sekta za afya na elimu, kutenga fedha kwa ajili ya huduma za lishe na mapambano dhidi ya maambikizi ya VVU na UKIMWI na kuwekeza katika miradi yenye mwelekeo wa vyanzo vya mapato hasa katika sekta ya kilimo na biashara.

Halmashauri imezingatia mwongozo wa taifa wa kutenga bajeti  kwa ajili ya makundi maalum ikiwa walemavu asilimia 2, maendeleo ya wanawake 4 % na vijana 4%.

Hata hivyo alimalizia kuwasilisha bajeti mbele ya baraza la madiwani kwa kutoa mchanganuo wa matumizi ya makusanyo ya ndani, ikiwa  Tsh 813,225,758 zitatumika katika   miradi ya maendeleo itakayotekelezwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020, na tsh 1,219,838,638 kwa matumizi mengineyo. “lakini bajeti yetu ni pungufu kwa asilimia 15.5 ya mwaka 2018/2019 kutokana na kutojumuishwa kwa bajeti ya maji na baadhi ya program kama SEDEP, ASDP na LGCDG kumalizika muda wake” alisema kaimu afisa mipango.

Baraza la madiwani walipokea rasimu ya bajeti iliyowasilishwa na kuijadili na kutoa Baraka ili iwasilishwe katika ngazi nyingine za maamuzi kwa ajili ya utekelezaji,na kuomba serikali kuwasilisha fedha za miradi kwa wakati ili kukamilisha miradi pendekezwa kwa wakati.

Aidha mwenyekiti wa halmashauri ya Tunduru Ndg Mbwana Mkwanda Sudi aliwataka madiwani kushiriki katika zoezi la usimamizi na ukusanyaji wa mapato na  kuibua vyanzo vipya vya mapato ili kuweza kufikia lengo la serikali la kila halmashauri kukusanya asilimia 80.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.