Uwajibikaji na ufanisi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo umeendelea kupewa kipaumbele Wilaya ya Tunduru baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, ndug. Chiza Marando, kuzindua rasmi mikataba kwa wasimamizi wa miradi inayoendelea kutekelezwa ndani ya Halmashauri.

Uzinduzi wa mikataba hiyo umefanyika leo katika kikao maalum kilichofanyika Ofisi ya Mkurugenzi, kikihusisha wasimamizi wote wa miradi ya maendeleo kutoka sekta mbalimbali ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.
Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mkurugenzi Mtendaji amesisitiza umuhimu wa wasimamizi wa miradi kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia masharti ya mikataba waliyopewa, kwa kuzingatia viwango vya ubora, muda uliopangwa na matumizi sahihi ya rasilimali za umma.

Hatua ya kuanzishwa kwa mikataba hiyo inalenga kuimarisha uwajibikaji, kuongeza uwazi na ufanisi katika utekelezaji wa miradi, pamoja na kuhakikisha thamani ya fedha kwa miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa kwa manufaa ya wananchi wa Wilaya ya Tunduru.
Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru inaendelea kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha miradi ya maendeleo inakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyokusudiwa, ili kuleta tija na kuboresha maisha ya wananchi.
Halmashauri ya Wilaya Tunduru
Anuani ya Posta: 275, TUNDURU
Simu: + 255-025-2680004
Simu ya Nununu:
Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz
Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.